ASENGA MBUNIFU WA JIKO LA KIKAPU

 Deograsias Asenga akiwa ameshika jiko la kikapu pamoja na malighafi inayotumika kutengeneza jiko hilo.

Peter Akaro

BADO watanzania wanashahuku ya kubuni vitu ambavyo vitainuisha jamiii na kuiletea unafuu wa maisha  kwa siku za usoni.

Leo tupoona kijana Deograsias Asenga ambaye amebuni jiko la kikapu ambalo linalitumia joto kiasi la sufuria kuivisha chakula.

Jiko hili linapika kwakutumia joto pekee yake ambalo sufuria hutokanalo wenye moto wa awali ambao unaweza kuwa wa kuni, mkaa, umeme na  hatagasi.

Kabla ya kufikambali zaidi ningependa tuangalie jinsi jiko hilo linavyotengezwa ilikupata picha ya kile nina chozungumzia.

Asenga anasema kwanza unatakiwa kuwana kikapu ambacho kinaweza kuwa cha mianzi au ukili,kitamba cheusi na malighafiya ‘Styrofoam’.

“Hizi malighafi hutumika kubebea runinga, redio, na vifaa vya kieletroniki ambazo tunakuwa tumeshazisaga, kisha zinachanganywa na mafuta ya kikapu na zikishalowa tunaanika kwa muda wa dakika 20.

Anasema baada ya hapo unaziingiza kwenye karatasi ambazo ni laini sana kisha unaziingiza ndani ya kikapu ambapo ile karatasi itatakiwa izunguke kikapu chote na kila sehemu kuwena hizo‘Styrofoam’.

“Hili karatasi inauzwa sh. 2,000, unakuja kuikata vipande vipande kwa kulingana na ukubwa wa kikapu, mwishoni unashikilia kwa nje ili kupata nafasi ya kuja kuingiza zile malighafi kwa uwiano.

Ukisha maliza unachukua kilekitambaa cheusi unashonea juu lilekaratasi, ukishamaliza unakunja kisha unashonea ili kuondoa ule muonekano wa kipapu cha ukili au mianzi.

Asenga anasema anaweka kitambaa cheusi kwasababu kina uwezo wa kuakisi na kuifadhi joto kiurahisi.

Baada ya hatua hiyo inafuata utengenezaji wa ufuniko wa jiko ambao  unachukua mfuko wa nailoni (malboro), kisha unasaga tena‘Styrofoam’na kuzichanganya na yale mafuta, baada  ya hapo unaziweka  ndani ya huo mfuko na kuushona.

“kuuchukua huu mfuniko kama ulivyo na kuuweka juu ya jiko nikitu ambacho haikiwezekani, kwa hivyo unachukua kitambaa cheusi na kukishona, kisha unashusha ule mfuko na kuingiza ndani yake na baadae unakuja kushona lile eneo ulilopitisha  ule mfuko.

“Hadi kufikia hapa jiko linakuwa tayari kutumika bila shida yoyote,” anasema.

Jinsi lina vyotumika

“Hili jiko linatengemea jiko lingine ambalo litaipa sufuria joto na kile kilichopo ndani kwa muda ndipo ile sufuria ina hamishiwa huku ili kuendelea, kwa mfano unapika ubwabwa, unachemsha maji katika jiko lingine na kuweka vitu vyote vinavyohitajika baada ya  muda unatoa kwenye lile jiko la mwanzo, na kuweka kwenye kapu lako ambalo sasa ndio jiko na kufunika na baaada ya dakika  20 ubwabwa wako utakuwa umeivakabisa,” anasema.

Anasema jiko hili lina weza kuhifadhi joto kwa masaa nane hadi 12, na mtu anaweza kutembea nalo huku anapika bila shida yoyote.

“Kama unapika maharage, utayachemsha kwenye jiko la awali kwa dakika 30, baada ya hapo utaamishia kwenye jiko la kikapu na baadae ya lisaa limoja na dakika 20 maharage yana kuwa yameiva vizuri na kulainika.

“Na unapokuwa umeweka maharage yakondani, ukisikiliza kwanje utasikia kamajiko linatoamtetemeko kwasababu joto kwa asilimia kubwa linakuwa limemezwa na zile malighafi na nailoni na mvuke unaendelea kubaki ndani nakuendelea kuivisha. 

“Mvuke hauwezi kuharibu kitambaa kwasababu hizimalighafi zinahifadhi joto na kuachia kidogo kidogo,” anasema.

Anasema ‘Styrofoam’ zinapokuwa zinachanganya na mafuta huwa zinatabia ya kufyonza na kutanuka, ila zinapokuwa zina chomwa najoto la sufuria zinaachilia na kuwa ndogo zaidi, hivyo kuleta kuwana uwezo mkubwa zaidi wa kupika na joto linapokuwa linazidi zinakuwa kama gundi.

Asenga anaongeza kuwa baadae zikipoa zinarudia katika hali yake ya kawaida.

“kinachofanya kazi asilimia kubwa ni haya mafauta, na ukitumia bila mafuta jiko litapika lakini halitakuwa na ubora …litapika kwa siku kadhaa ingawa hili jiko linaweza kukaa zaidi ya miaka 10,” anasema.
 Mafanikio na ushauri

Asenga anasema mwaka jana yeye na wenzake walichukuliwa na serikali hadi Mtwara katika kijiji cha Nanyambe kufundisha watu namna ya kutengeneza jiko la kikapu.

Anaongeza kuwa haikushia hapo bali walienda hadi Lindi Mjini ambako kulikuwa na maonyesho ya Nane Nane na hapo wakawafundisha watu pia.

“Ingawa walitusifu kwa kufanya kazi nzurii ila bado mchango wetu haujatambuli wa rasmi na serikali, bado kuna mlologo mrefu hadi kutufikia.

“Kwa mfano sisi tulipelekwa na Halimashauri ambao wangetakiwa kukaa nasisi kwasababu wao ndio wanajua kiu ya wananchi ni nini na watusaidie ili tuweze kujikwamua kiuchumi, si hadi kuongoja serikali kuu,” anasema.

Mbunifu huyu anasema huu ndio wakati ambao serikali ingetakiwa kuwasaidia kwasababu wameshaona uwezo wao hata kwa kufundisha wengine, na endapo likitekelezwa hilo nirahisikwa wao kuboresha na kubuni zaidi.

Wasifu wake

Anasema kiwango chake cha elimu ni darasa la saba ambapo alihitimu elimu hiyo mwaka 1997 katika Shule ya UaRombo Kilimanjaro.

“Baada ya hapo wakati nikisubiri matokeo nikajiunga na shule ya ufundi Mahida Rombo, na matokeo ya darasa la saba yalipotoka hayakuwa mazuri hivyo nikaamua kuja Dar es Salaam.

“Mwaka 1999 nikanza kufanya biashara ya vya kula hadi 2007, na mwaka uliofuata nikaanza tena shule ya ufundi wa magari katika  Chuo fulani na mwaka 2009 ni kaenda kujiunga naVeta Chang”ombe ambapo ni liihitimu mwaka huo huo,” anasema.

Mbunifu  huyu anasema  ufundi wake uliishia daraja la pili kwa kuwa alishindwa kufaulu mitihani ya kujiunga na daraja la kwanza.

“Baada ya hapo nikawa nafanya kazi kwenye gereji lakini kazi zikawa hamna fedha ninayo pata haitoshi matumizi ya kifamilia.

“Lakini baadae nikaona hapana, nikaamua kujiingiza katika  ubunifu  na ujasiriamali ambao ndio unaendesha maisha yangu hadi sasa,” anasema.

Contact: 0755 299596

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.