MKURUGENZI MKUU WA NBS AFANYA KIKAO NA WAFANYAKAZI WA OFISI HIYO, NA KUWATAKA KUFANYA KAZI KWA BIDII.

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akizungumza wakati wa kikao cha wafanyakazi wa ofisi hiyo, kilichofanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. Katika kikao hicho, Dkt.Chuwa amewataka wafanyakazi hao kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kuboresha zaidi upatikanaji wa takwimu rasmi nchini.

Kaimu Mkurugenzi wa Utawala, Fedha na Masoko, Lilian Karumuna wa Ofisi ya Takwimu akifafanua jambo wakati wa kikao cha wafanyakazi wa ofisi hiyo, kilichofanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.

 Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania Tawi la Ofisi ya Taifa ya Takwimu (TUGHE) Raya Mikidadi akifafanua jambo wakati wa kikao cha wafanyakazi wa ofisi hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. 

 Baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi ya Takwimu wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu Dkt. Chuwa (hayupo pichani) wakati wa kikao cha wafanyakazi wa ofisi hiyo, kilichofanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. 

Baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi ya Takwimu wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) wakati wa kikao cha wafanyakazi wa ofisi hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO).

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.