SERIKALI IMEOMBWA KUZIACHA TAASISI ZA DINI KUTOA HUDUMA KWA UTARATIBU WALIOJIWEKEA.


Na Mwandishi Wetu, Iringa.

SERIKALI imeombwa kuziacha Taasisi za dini kuendelea kutoa huduma mbalimbali ikiwamo elimu na afya kwa utaratibu waliojiwekea badala ya kuzilazimisha  kusajili na kuendesha huduma hizo kibiashara jambo ambalo ni kinyume na malengo ya taasisi hizo.

 Rai hiyo imetolewa juzi na Paroko wa Parokia ya Nyabula Jimbo la Iringa, Padre Emil Kindole, kwenye kongamano la vijana wa Vikaria ya Consolata lenye jumla ya parokia 11 kutoka jimbo la Iringa.

Kindole alisema kuwa “serikali inawaumiza  pale ambapo inatutaka sisi kama kanisa tufanye biashara, hatujazoea biashara wala biashara hatuijui kwa mfano St.Thomas iwe ni biashara  tukate leseni ya biashara sisi hatuwezi afya na shule ni huduma ukisema ni biashara lazima tukae upya tujipange na tuseme tutaiendeshaje kibishara.”alisema Padri Kindole.

Naye  Pascal Mahondo ambaye  ni katibu wa Vikaria ya Consolata alisema kuwa  kongamano hilo  limewekwa kwa lengo ya kuwaamsha vijana kufanya uenezi wa injili takatifu kazi iliyoasisiwa na wamisionari kutoka ulaya miaka150 iliyopita ambapo vijana wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kuihubiri injili ili kuhakikisha taifa linaendelea kuwa na amani ambayo ni kichocheo cha maendeleo.


 Kwa upande wake mgeni rasmi wa kongamano hilo ambaye ni  Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Rita Kabati alisema wabunge wa mkoa wa Iringa wameanza kushughulikia changamoto ya za miradi ya huduma za mashirika ya dini ili kuhakikisha huduma hizo zinaendelea kuwapo kwa lengo la kuisaidia jamii kama ilivyo dhamira ya mashirika hayo.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.