NBS YAKUTANA NA WATAALAM WA MFUMO WA TAARIFA ZA KIJIOGRAFIA (GIS) UTAKAOTUMIKA KUPUNGUZA GHARAMA ZA UKUSANYAJI TAKWIMU MBALIMBALI NCHINI.

 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akizungumza wakati wa kikao cha pamoja baina ya wataalam kutoka Kampuni ya esri-  inayojishughulisha na kutoa huduma za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS), walipokutana leo Jijini Dar es Salaam ili kujadili namna mfumo huo unavyoweza kutumika wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu mbalimbali nchini. Kulia ni Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Shirila la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA Tanzania) Dkt. Hashina Begum. 



 Mtalaam kutoka kampuni ya esri - inayojishughulisha na kutoa huduma za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS), Bi. Linda Peters akielezea jambo wakati wa kikao baina ya wataalam kutoka Kampuni hiyo na Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)  leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni wataalam kutoka Kampuni hiyo Bw. Patrick Kipchumba na Mhandisi Anthony Gakobo.



 Baadhi ya wataalam kutoka Kampuni ya esri - inayojishughulisha na kutoa huduma za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS), wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) walipokutana leo Jijini Dar es Salaam ili kujadili namna mfumo huo unavyoweza kutumika wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu mbalimbali nchini.



 Mtalaam wa Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS) Anthony Gakobo akionyesha moja ya kifaa kinachotumika katika kuhakiki uhalisia wa taarifa za kijiografia mbele ya Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni watalaam wa mfumo huo  Patrick Kipchumba na  Linda Peters.


 Mshauri wa Masuala ya Kitakwimu kutoka Benki ya Dunia – Tanzania,  Elizabeth Talbert akifafanua jambo wakati wa kikao cha pamoja baina ya wataalam kutoka Kampuni ya esri-  inayojishughulisha na kutoa huduma za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia (GIS) na menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ili kujadili namna mfumo huo unavyoweza kutumika wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu mbalimbali nchini.


Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa, (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi kutoka UNFPA, Benki ya Dunia – Tanzani , watalaam kutoka Kampuni ya esri inayojishugulisha na kutoa huduma za Mfumo ya Taarifa za Kijiografia (GIS) pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)  mara baada ya kumaliza kikao kujadili namna mfumo wa GIS unavyoweza kutumika wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu mbalimbali nchini.

(Picha zote na Frank Shija – MAELEZO)


Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.