SOKO LA SAMAKI KUNDUCHI WABUNI NJIA YA KUWADHIBITI WAVUVI HARAMU.


Na Enles Mbegalo

UONGOZI wa Soko la Samaki Kunduchi, Dar es Salaam limeunda Kikundi cha  Ulinzi Shirikishi cha Pwani na Baharini  (BMU), kwa lengo la kudhibiti uvumi haramu.

Akizungumza na mwandishi wa blog hii, mmoja wa viongozi wa soko hilo, Ramadhani Ali, alisema kikundi hicho cha watu 15 kitafanya doria kwenye fukwe  za bahari kwa masaa 24 ili kuwadhibiti wavuvi hao pamoja na wachafunzi wa mazingira ya fukwe hizo.

“Ulinzi huu  wa baharini utasaidia sana kuwaokoa baadhi ya samaki ambao wameaza kupotea kabisa baharini na tutagundua ni samaki wapi hawapatikani kwa sasa na kipindi cha nyuma walikuwa wanapatikana,”alisema Ali

Pia, alisema  pamoja na serikali kupiga vita uvuvi huo ila inatakiwa kuwasaidia wavuvi hao vifaa vya kisasa kwaajili ya kuvitumia katika shughuri zao za uvuvi.

Hata hivyo, alisema soko hilo limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimba ikiwamo usalama mdogo kwa wavuvi kwani  wamekuwa wakitishiwa maisha yao na vijana wasiojishughurisha na shughuri yeyote kwenye soko hilo.

“Kulingana na hali iliyopo sasa kila mtu anatakiwa kufanya kazi ila vijana wengi wamekuwa wakikimbilia sehemu ya wavuvi na kutojishughurisha na kazi yeyote,”

Pia alisema soko hilo linakabiriwa na changamoto ya ukosefu wa vyoo na kupelekea baadhi ya wavuvi wanaoishi kwenye eneo hilo kujisaidia pembezoni ya fukwe za bahari.



Baadhi ya wavuvi kwenye soko hilo, wakiandaa boti kwaajili ya shughuri za uvuvi.
Mfanyabiashara akiandaa dagaa kwa ajili ya kukaanga na kuuza katika Soko hilo
Kiongozi wa Soko hilo, Ramadhani Ali akionesha  Dema ambalo hutumika  kwa ajili ya kuvua samaki wakubwa.
Bado wagaangaji wa kitoweo cha samaki wakiwa wanatumia kuni kwa ajili ya shughuli zao kwa wateja.
Baadhi ya vitendea kazi za uvuvi zikiwa zimewekwa kwa ajili ya ukarabati.
Baadhi ya Nyumba wanazoishi wavuvi wakiwa katika shughuli zao za kila siku.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.