CUBA IKO TAYARI KUTUMIA UTAALAMU NA FEDHA, KUONA ZANZIBAR INAFIKIA MAENDELEO.


Balozi Mpya wa Cuba Nchini Tanzania Profesa Lucas Domingo Hernandez  Polledo  Kushoto akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofika kujitambulisha rasmi hapo Vuga Mjini Zanzibar.

 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi zawadi ya Mlango Balozi Mpya wa Cuba Nchini Tanzania Profesa Lucas Domingo mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.

Balozi Seif kati kati akiwa katika picha ya pamoja na Mtaalamu wa Benki ya Dunia anayesimamia Kampuni ya MIGA Bwana Yasumitsu Himeno    wa kulia yake baada ya kufanya mazungumzo Ofisini kwake kuhusiana na miradi ya Uwekezaji.




Na Mwandishi wetu, Zanzibar

JAMHURI ya Cuba imesema iko tayari kutumia Utaalamu, Maarifa, Uzoefu na  fedha ili kuona  Zanzibar inafikia maendeleo makubwa ya Wananchi wake  Kiuchumi kama ilivyofikia Nchi hiyo.

Balozi Mpya wa Cuba Nchini Tanzania, Profesa Lucas Domingo Hernandez Polledo, alisema hayo wakati wa mazungumzo yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, alipofika kujitambulisha rasmi hapo Vuga Mjini Zanzibar.

Profesa  Domingo alisema Cuba haina sababu ya kutoiunga  mkono Zanzibar katika harakati zake za kuimarisha uchumi kutokana na Historia ya muda mrefu iliyopo baina ya Visiwa hivyo.

  “Wananchi wa Jamuhuri ya Cuba tayari wameshaonyesha ukarimu mkubwa kwa wenzao wa Zanzibar na natolea  mfano mafungamano ya Sekta ya Afya yalivyoimarika na kupata mafanikio makubwa hasa kilipoanzishwa  Chuo cha Madaktari kinachosimamiwa na wataalamu wa Nchi hiyo,”alisema na kuongeza

“Wakati umefika kwa Mawaziri wa pande hizi mbili rafiki kukaa pamoja kujadili namna viongozi hawa wanavyoweza kushirikiana katika mambo yanayoonyesha kufanana katika utekelezaji  wa pamoja,”

Alisema vikao hivyo vinaweza kuibua mambo ya msingi ndani ya sekta ambazo kwa kiasi kikubwa zinaweza kusaidia kwenye miradi mbalimbali ikiwamo  Kilimo.

Pia amemuahidi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa kipindi chake cha utumishi wa Kidiplomasia  atazingatia zaidi kuimarisha uhusiano wa Kihistoria wa pande hizo mbili.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameendelea kuishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Cuba kwa juhudi inazochukuwa za kuiunga mkono Zanzibar katika Sekta ya Afya ambayo tayari imeshazalisha Madaktari wazalendo wasiopungua 50 kupitia Chuo cha Madaktari kinachosimamiwa na Wataalamu wa Nchi hiyo.

Alisema moja ya fanikio kubwa lililopatikana na ubanaji wa matumizi ya Serikali ambayo mwanafunzi Mmoja wa kada ya Udaktari angelazimika kulipitia masomo yake kwa zaidi ya Dola za Kimarekani 17,000 elfu.

Wakati huo huo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikutana kwa mazungumzo na Ujumbe wa Wataalamu wa Benki ya Dunia wanaojishughulisha na kusimamia miradi ya uwekezaji kupitia Kampuni ya MIGA yenye Makao Makuu yake Nchini Japan.

Mazungumzo hayo ambayo  pia yalimjumuisha  Balozi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Japan Balozi Mathias Chikawe aliyeambatana na Ujumbe huo yalifanyika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Bwana Yasumitsu alisema ipo miradi mingi iliyoanzishwa katika Mataifa mbali mbali yenye uwanachama wa Benki ya Dunia ambayo hupata mikopo chini ya Makampuni yanayodhaminiwa na Benki hiyo yanayotozwa gharama za asilimia 50% ya mradi wanaoutekeleza.

Alitoa mifano ya miradi hiyo kuwa ni pamoja Hospitali kubwa zenye uwezo wa kuhudumia wagonjwa katika Mikoa Mikoa na Miji Mikubwa, majengo ya Vyuo Vikuu, Viwanja vya Ndege, miradi ya Ulinzi na hata miuondombinu ya Bara bara.

Naye, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif  ameushauri Uongozi wa Kampuni hiyo ya MIGA kuangalia uwezekano wa kuunga mkono Mpango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wa kutaka kuziimarisha Hospitali Mbili za Mikoa ya Kukisini na Kaskazini za Kisiwa cha Unguja.





Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.