Umoja wa Gereji Tegeta waiomba Serikali kuwamilikisha eneo

Na Enles Mbegalo

UMOJA wa Mafundi Gereji Tegeta, jijini Dar es Salaam,wameiomba serikali kuwamilikisha eneo hilo, ili waweze kufanya kazi kwa weredi na kuboresha miundombinu ya eneo hilo.

Akizungumza na mwandishi wa habari jana, Mjumbe wa Miundombinu kwenye gereji hiyo, Mei Hiza alisema changamoto ya miundombinu  mibovu ya gereji hiyo  sio mizuri na imewafukuzia baadhi ya wateja wao.

“Kutokuaminishwa eneo hili la magereji limepelekea sisi kushindwa kufanya kazi kwa weredi na kuboresha miundombinu hii kutokana na kutokuwa na uhakika na eneo hili ambalo tumewekeza,”alisema Hiza

Aliongeza kuwa “Kama serikali wakituaminisha na kutumilikisha tutafanya kazi zetu kwa weredi tunashindwa kufanya hivyo kutokana na  migogoro ambayo ilikuwepo kwenye eneo hili tangu mwaka mwaka 2013,”

 Hiza lisema kutokana na kazi wanazozifanya kwenye gereji hiyo ikiwamo kutengeneza vipuri vya viwandani, makampuni na watu binafsi wanaiomba serikali iwaangalie kwa kuwapa kazi mbalimbali ambazo zinatengenezwa kwenye gereji hiyo.

Aidha eneo hilo ambalo liliaza mwaka 2006 likiwa na mafundi gereji 280 ambapo hadi sasa wamefikia zaidi ya 6000.


Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.