TAKUKURU IRINGA YAOKOA ZAIDI YA SH. MILIONI 11 ZILIZOKUWA MALIPO HEWA KWENYE ELIMU.

Na Mwandishi wetu, Iringa

TAASISI  ya kupambana na rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Iringa imeokoa jumla ya Sh. Milioni 11,921,800 ambazo zilikuwa ni malipo hewa kutoka idara ya elimu katika kituo cha Ilula.

Akizungumza na mwandishi wa blog hii, hivi karibuni ofisini kwake, Evarist Shija kwa niaba ya Mkuu wa Takukuru mkoani hapa wakati akitoa taarifa ya utekelezaji kazi wa Takukuru kwa kipindi cha mwezi  Julai 2016 hadi Machi 2017.

Shija  alisema kuwa taasisi hiyo imepokea malalamiko 98 ya rushwa na 16 kati ya hayo yamefunguliwa majalada ya uchunguzi,malalamiko 15 yanafanyiwa uchunguzi wa awali huku wakifunga malalamiko 67 yaliyoshindwa kuthibitisha Makosa ya rushwa.

Pia alisema kuwa taasisi hiyo imefikisha mahakamani kesi saba kwa makosa mbalimbali ya rushwa,na kwa kesi hizo saba ofisi hiyo inafikisha jumla ya kesi tisa za makosa ya rushwa zinazoendelea mahakamani baada ya kesi tano kutolewamahakamani kwa kesi mbili kushindwa kuthibitisha makosa ya rushwa na kesi tatu kuwatia hatiani watuhumiwa.

Alisema  katika kesi hizo, zinahusu watuhumiwa kutoka idara mbalimbali ikiwamo utawala,Afya,Fedha na ushirika (mtendaji kata uhambingeto,afya wafamasia wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi pamoja na ushirika).

Aliongeza kuwa idara zinazoongoza kwa kulalamikiwa kwa rushwa ni TAMISEMI ambapo ofisi hiyo imepokea malalamiko 32 kutoka tamisemi,idara za polisi 13 na elimu 11 na kuongeza kuwa yapo malalamiko kutoka idara za ardhi na mahakama.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.