WADAU WAMEOMBWA KUSAIDIA WATOTO YATIMA.


 Na Enles Mbegalo

MKURUGENZI wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Amani Orphanage, Magreth  Mwegalawa,kilichopo Bagamoyo Mkoa wa Pwani amewaomba wadau mbalimbali kujitoa  kwa moyo katika kusaidia watoto hao.

Hayo aliyasema leo mkoani humo wakati wa ufunguzi wa mabweni mawili ya kulala watoto wa kiume na wakike kwenye kituo hicho.

“Kutoa ni moyo nawaomba wadau mbalimbali wajitoe kwaajili ya watoto wasiojiweza kwani kufanya hivyo ni kupata dhawabu kwa Mwenyezi Mungu,”alisema Mwegalawa.

Alisema changamoto zilizopo kwenye kituo hicho ni za kawaida ikiwamo kukosa chakula, vifaa vya shule hasa kwa kipindi cha miezi ya kuanza shule na kufungu.

Aliongeza kuwa kituo hicho kilianza na watoto wawili ambapo hadi sasa wamefikia watoto 38.

Pia alisema kituo hicho kinapokea watoto hao kuanzia kuzaliwa.

MKURUGENZI wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Amani Orphanage, Magreth  Mwegalawa,akiwa ameongozana na Mchungaji wa Kanisa la Lutherani (KKKT) Usharika wa Boko jijini Dar es Salaam,Hermani Mkini, baada ya kufanya uzinduzi wa mabweni hayo Bagamoyo.

 Mchungaji Mkini na Mkurugenzi wa Kituo hicho Magreth akiwa kwenye picha ya pamoja na watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho.

Baadhi ya wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali waliohudhulia hafla hiyo leo.



 Mchungaji Hermani Mkini akiwa ameketi kabla ya kuaza uzinduzi wa mabweni hayo. (PICHA ZOTE NA MAISHA NI HABARI BLOG).
   



Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.