EVOD, AWAOMBA WANANCHI KUSHIRIKIANA KUTENGENEZA BARABARA YA NGORONGORO.


Na Enles Mbegalo

MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Pwani Manispaa ya Kinondoni Dar es Salaam,Evod Rashid, amewaomba wananchi wa mtaa huo kushirikiana kutengeneza mitaro ya barabara ya mtaa wa ngorongoro ili kuepuka usumbufu uliopo kwenye barabara hiyo.

Akizungumza  leo na mwandishi wa blog hii, Rashid alisema barabara hiyo, imekuwa ikitumika na watu wengi ila kwa kipindi hiki cha mvua imekuwa ikileta usumbufu kutokana na maji kutuwama kwenye barabara hiyo.

“Kila kitu kinahitaji ushirikiano kwa pamoja tukishirikiana na wananchi wangu tunaweza na nawaomba wasife moyo tushirikiane kutengeneza mitaro ya kupitisha maji eneo hili ili tuepukane na usumbufu huu ambao unatokea hasa kwa  kipindi hiki cha mvua,”alisema Rashid

Rashid, alisema kuna wadau wametoa greda kwaajili ya kutengeneza barabara hiyo, ila kunahitajika fedha nyingi sana kwaajili ya kuweka mitaro itakayokuwa inapitisha maji na kupeleka baharini.

 Mwenyekiti Evod, akiendelea kuonyesha eneo la barabara hiyo linalohitaji ukarabati.
 Mfanyabiashara wa mbogamboga akipita katika eneo hilo akisaka wateja.
Baadhi ya wananchi wakipita kwa tabu katika eneo la barabara hiyo. (PICHA ZOTE NA MAISHA NI HABARI BLOG)....

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.