WATANZANIA WATAKIWA KUWA WAVUMILIVU NA SIO KUTAFUTA NJIA YA MKATO.

 Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

WATANZANIA, wametakiwa kuwa wavumilivu kwa jambo lolote wanalolifanya na sio kutafuta njia za mkato kufikia malengo yao ambazo zitawafikisha pabaya.

Wito huo umetolewa leo na Askofu  Mkuu wa Dayosisi Kuu ya Dar es Salaam na Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania (KMUT), Emmaus Mwamakula,  katika kituo cha Ibada cha Mliman City Worship Centre (MCC).

“Watanzania tuwe wavumilivu na sio kutafuta njia za mikato kwenye maisha yetu kwani jambo lolote lile jema  hufanywa kwa bidii na sio kutumia njia za mkato,”alisema na kuongeza

“Tujifunza uvumilivu kama neo  la leo lilivyosema, tuogope mambo ya mkato kwani mambo haya yatatupeleka mahali pasipo pazuri,”
 “Mfano katika nchi yetu siku hizi  za karibuni Rais Dkt. John Pombe Magufuli alikabidhiwa Ripoti  na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) na kubaini  mambo mbalimbali ikiwamo baadhi ya watumishi wa umma kugushi vyetu  na walifanya haya kwa kupitia njia ya mkato ili waweze kufika bila kugundua matatizo ya baadaye,”

Aidha,Askofu Mwamakula, alisema wamefungua  kanisa ndani ya Mlimani City kwaajili ya kuwafikia watu wote bila kuangalia dini zao.

Naye Mtumishi ambaye pia ni Mtaalamu wa Mionzi ya Tiba kutoka Hospitali ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road jijini Dar es Salaam, Steven Mkoloma, ambaye pia  alihubiri kwenye ibaada hiyo alisema katika maisha  unatakiwa kupambana na haijalishi upo katika mazingira gani Mungu anamaagano na wewe.

Mkoloma, alisema mipango na bidii kwenye maisha itakupeleka
 kwenye utajiri ila  njia za mkato zitakupeleka kwenye umasikini.

Waumini waliohudhulia kwenye idaada hiyo  katika kituo cha maombi cha Mlimani City jijini Dar es Salaam leo 30/4/2017 .
Waumini wakiimba  nyimbo katika kipindi cha kusifu kilichoongozwa na Mwimbaji wa Injili Tanzania na Muingizaji wa Bongomovie, Silvanus Mumba, akiwa na waimbaji wengine watano  wa nyimbo za injili  hawapo pichani.

Waumini wakiendelea kumtukuza Mungu katika kipindi cha sifa katika kituo cha Ibada cha Mlimani City.
(PICHA ZOTE NA MAISHA NI HABARI.)

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.