MWENYEKITI AIOMBA SERIKALI KUOKOA KAYA 50 ZILIZOZINGILWA NA MAJI.


Maji yakiwa yametuama katika nyumba za wakazi wa eneo la Bunju A Kirungule jijini Dar es Salaam jana, yakiwa na madhara kwa Wananchi waishio hapo kiafya.


Na Enles Mbegalo

MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Bunju A Kirungule, Seif Sitambuli ameiomba serikali kuokoa maisha ya kaya zaidi ya 50 ambazo nyumba zao zimezingilwa na  bwawa la maji zaidi ya miaka mitatu jijini Dar es Salaam.

Aidha, ameiomba   serikali kutoa maeneo  salama kwa wananchi hao ili kuokoa maisha yao kwa ujumla.

“Ninaiomba serikali iangalie namna ya kuzisaidia kaya hizi kwani hali  iliyopo kwenye maeneo haya inaweza kuleta maafa zaidi pamoja na kutokea  magonjwa ya milipuko,”alisema

Alisema pia athari kubwa  inayoweza kujitokea kwa wakazi hao hasa kwa kipindi hiki  hiki cha mvua pia  serikali ingeliangalia hilo ili waweze kuepusha madhara hayo kabla hayajatokea.

“Licha ya serikali kuendelea kutoa misaada  mbalimbali lakini tatizo hilo bado ni kubwa hivyo kupewa kwao viwanja ambavyo viko maeneo salama ingesaidia zaidi,”alisema Sitambuli

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.