ASILIMIA 10 YA WANAUME WAPO HATARINI KUPATA TEZI DUME .



Na Enles Mbegalo

ASILIMIA 10 ya wanaume waliofikia umri wa miaka 40 wapo hatarini kupata ugonjwa wa tezi dume.

Akizungumza na mwandishi wa blog hii , Mtaramu wa Madawa na Tiba ( PharmD),  kutoka Hospitali ya Sanitas jijini Dar Es Salaam, Doctar Sajjad Fazel alisema ugonjwa huo nirahisi kuupata kadri umri unavyoongezeka.

“Asilimia 10 ya wanaume waliozidi  umri wa miaka 40 na waliozidi miaka 60 wanapata tezi dume na kadri umri unavyoongezeka unapata tezi dume,” alisema na kuongeza

“Tenzi dume ni kiungo kinachopatikana chini ya kibofu cha mkojo na kinazunguka milija ya mikojo,”

DK. Fazel alisema dalili ya tezi dume ni kukojoa mara kwa mara, kuchukua muda mrefu ukitaka kukojoa,mkojo kutotoka kikamilifu,kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa.

Alisema dalili nyingine ni kupata maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa na ikifikia hatua za mwisho za tezi dume inatoka damu kwenye mkojo.

“Ugonjwa huu ukitambulika mapema unaweza kutibika kwa kutumia dawa na kufanyiwa upasuaji,”alisema na kuongeza

“Kama mtu anasaratani ya tezi dume na haijagundulika inasambaa kwenye viungo vingine vya mwili wake na mwisho wake anafariki na kama unayo na hujapima ni hatari zaidi kama haijagundulika unaweza pata saratani ya ini na kibofu cha mkojo,”

Aliwashauri wanaume wote waliozidi miaka 35 wanashauriwa kupima kila baada ya miezi miwili.


Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.