NEMC YAWATOZA FAINI YA SH. MILIONI 20 WAWEKEZAJI WA KILIMO NA MIFUGO.


Na Mwandishi Wetu, Kilolo
BARAZA  la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), imewatoza faini ya jumla ya sh. milioni 20 wawekezaji wawili wa kilimo na ufugaji Wilayani Kilolo kwa makosa ya kuendesha shughuli zao bila kufanya tathmini ya uharibifu wa mazingira.

Adhabu hiyo imetolewa na mwanasheria wa NEMC, David Kongola baada ya kutembelea mashamba ya wawekezaji hao na kubaini kasoro kubwa za kimazingira na kuhatarisha usalama wa vyanzo vya maji.

Kongola alisema kuwa “Sasa adhabu yao hawa  sisi tunatoza Mil.10 kwa kila mmoja kwa kufanya hii shughuli bila ya kuwa na (IAA) Certificate na hiyo ipo wazi kwamba kifungu no.184 kinasema isizidi Mil.50 na sisi tun asema kwamba Mil.10 na tutawaletea invoice kwa kuendesha biashara yako bila ya kuwa na cheti cha tathimini ya mazingira.”alisema Kongola

Adhabu ya NEMC imeyakumba mashamba ya mifugo ya Tomy Dairies na  la Ndoto yaliyopo kwenye kata ya Ihimbo ambapo mwanasheria wa NEMC alisema sheria lazima zifuatwe kulinda mazingira

Mmiliki wa shamba la Tomy pia alipewa muda wa wiki moja na kikosi kazi cha kuokoa ikolojia ya Mto Ruaha, kung’oa migomba iliyopandwa ndani ya eneo la chanzo cha maji cha Mto Ruaha Mdogo.

Akizungumza Wamoja Ayubu ambaye ni mjumbe wa kikosi kazi alisema kuwa eneo hilo halitakiwi kupandwa mazao hayo bali inatakiwa kupandwa miti ya asili ambayo itaendelea kutunza vyanzo vya maji na hivyo kumtaka kung’oa migomba yote kwa kuhesabu mita 60 kutoka usawa wa mto.

Hata hivyo wamiliki wa mashamba hayo walikiri mapungufu ingawa walisema kuwa hawakupewa mwongozo tangu awali.



“ Tumekiri kuwa na mapungufu hayo na tutajitahidi kuyarekebisha lakini pia sisi hatutaki kufanya jambo nje ya sheria.”Walisema wamiliki hao 
 
Aidha wamiliki hao wametakiwa kuvitunza vyanzo vya maji vilivyopo ndani ya maeneo yao kwa faida ya vizazi vijavyo ambapo  David Mginya ambaye ni mjumbe kikosi kazi alisema kuwa wanatakiwa kujenga miundombinu hiyo kwa lengo la kutunza vyanzo vya maji.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.