WANANCHI KIJIJI CHA MALIZANGU WAIOMBA SERIKALI KUWABORESHEA MIUNDOMBINU YA SKIMU YA UMWAGILIAJI.


Na Mwandishi Wetu, Iringa

WANANCHI wa Kijiji cha Malizangu Kata ya Mlowa Wilaya ya Iringa wameiomba serikali kuwajengea miundombinu ya skimu za umwagiliaji iliwaweze kuboresha kipato na uhakika wa chakula.

Wakizungumza na mwandishi wa blog hii kwa nyakati tofauti, kijijini hapo walisema kuwa mazao ambayo  walitarajia kuvuna msimu huu yamekauka baada ya mvua kuacha kunyesha.

“kilimo cha kutegemea mvua hakina uhakika tunaoimba serikali itujengee miundombinu ya skimu za umwagiliaji ili tuweze kuboresha kipato na uhakika wa chakula,”alisema

Nae, Marian Kamugishi, alisema kata hiyo mvua zimekuwa za shida,watu wanajuhudi za kulima lakini miundombinu hususani maji ya umwagiliaji hawana hivyo wanalima kilimo cha kubahatisha.

“Kilimo hiki hakina maana,tunadhani mkombozi wetu ni pale tunapopata maji ya umwagiliaji mfano skimu au tukavuna maji ya mvua kupitia mto mlowa na hali ya uchumi imekuwa ngumu kutokana na mvua kutokunyesha,”alisema

Kamugishi alisema kiujumla kijiji hicho kinarasilimali kubwa ambayo ni ardhi lakini mwaka huu kumekuwa na janga la kutokuwa na mvua.

Aliongeza kuwa mvua zimegoma zimeaza kunyesha mwezi wa pili, wananchi wamelima lakini mazao ndio kama hivyo na maji bondeni hakuna na kuishauri serikali iwasaidie kujenga banio mlimani kwa lengo ya kutunza maji kipindi ambacho mvua zimegoma kunyesha.

Kwa upande wake Ofisa Kilimo wa Kata ya Mlowa, Frank Kasumbi, alisema kuna hekta takriban 6,000 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji lakini changamoto ni kukosekana kwa rasilimali fedha kwa ajili ya kujenga miundombinu ya kutoa maji ya Mto Ruaha mdogo na kupeleka kwenye mashamba hayo.

“Bonde hili lina ukame na mvua ni za shida kitu ambacho kinapelekea wananchi wetu kukosa chakula na kipato kinazidi kushuka’alisema Kasumbi

Pia alisema changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi na ukame umeathiri uzalishaji na uapatiakanji wa chakula kwa wananchi wa kijiji cha Malinzanga kata hiyo.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Lulamso Kadaga alisema wananchi walishabuni mradi wa kutoa maji kutoka Mto Ruaha mdogo kwaajili ya umwagiliaji lakini mradi umeshindwa kukamilika kutokana na ukosefu wa rasilimali fedha.


Kadaga alisema kuwa “Kiujumla hali ya chakul kwenye kijiji change ni mbaya,kutoakna na mvua kutonyesha kwa wakati na ziliponyesha zilikatika mapema, mazao ya mahindi, alizeti, ufuta, mtama na mazao mengine yameshindwa kuvunwa kwa sababu ya ukame, njia pakee ya kujinusuru ni kuwa na kilimo cha umwagiliaji hasa mfereji.”

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.