Rusisye, apiga marufuku wananchi kuendelea kujenga eneo la ngema.

Na Enles Mbegalo

MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa Kunduchi , Richard Rusisye amewataka wananchi wa mji mpya eneo la kwa Mkorea kutoendelea kujenga wala kuishi eneo ambao lipo jirani na ngema ili kuondoka na hali ya kuhatari ya maisha yao.

Akizungumza na wakazi wa eneo hilo jana baada ya kwenda kuwapa pole wale walionusurika na kifo wakati ngema la eneo hilo lilipodondokea nyumba zao usiku.

“Ujenzi sambamba na eneo hili haturuhusu na tutakuja kuweka alama ya x na  baadhi ya nyumba  na watu watalazimika kubomoa nyumba zao na kuhama eneo hili kwani ni hatarishi kwa maisha yao,”alisema Rusisye

Aliongeza kuwa“miaka mitatu iliyopita lilidondoka ngema na kufukia watu wawili na mwaka jana nilikuja hapa nikawazuia  msijenge eneo hili kwani si salama kwa maisha yenu,”
Alisema uvumilivu umefika mwisho kwani yanapotokea majanga wanapoteza nguvu kazi ya taifa na marufuku mtu yeyote kuendelea kuchimba kokoto hapo.

Naye, Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi  Kawe  OCD, John Malulu, alisema wao kama viongozi watarazimika kuwaondoa watu waliojenga nyumba zao jirani na ngema hilo ili kuokoa maisha yao kwani maeneo hayo ni hatarishi.
Malulu, alisema  mfumo wa serikali unaaza na ngazi ya  mtaa ni lazima watu wachukue tahadhari.

Alitoa onyo kwa wananchi wanaoishi maeneo hayo kutogusa ngema hilo lililodondoka  kwa kuchimba kokoto na atakayebainika kufanya hivyo atachukuliwa hatua.

 “Msiguse hili ngema lililodondoka  kwa kuchukua mawe haya na tutaweka ulinzi hapa atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria,”

Naye, Renatha Kaijage, ambaye ni mmoja wa wahanga wa nyumba zilizondokewa na ngema hilo, alisema ngema hilo lilidondoka majira ya saa sita usiku ila yeye hakuwemo  eneo hilo.


 “ Majira ya  saa tano usiku dada aliniita niliporudi nilikuta ngema hili limedondokea nyumba ninayoishi, namshukuru Mwenyenzi Mungu maana ningekuwepo ningekufa,’

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.