OFISA MISITU KILOLO,ASHINDWA KUDHIBITI VYANZO VYA MAJI.


Na Mwandishi Wetu, Kilolo

OFISA Misitu wa  Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa ,Eugen Mwilafi, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kushindwa kutoa ufafanuzi wa kutosha kwa nini halmashuri hiyo imeshindwa kudhibiti kilimo kwenye vyanzo vya maji.

Hali hiyo imetokana na kukithiri kwa kilimo cha mabondeni maarufu kama vinyungu kando kando ya mito ya Mtitu na Lukosi inayotiririsha maji kwenye mito ya Ruaha Mdogo na Mkubwa.

 Ongezeko la kilimo cha vinyungu wilayani kilolo limebainishwa pia na viongozi wa wilaya hiyo mbele ya wajumbe wa kikosi kazi cha kuokoa ikolojia ya mto Ruaha Mkuu iliyoundwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu hivi karibuni wakati akiwa mkoani Iringa.

Akizungumza Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Asia Abdallah, alisema inatakiwa wanaolima kwenye vinyungu kutolewa kwenye eneo hilo na kupelekwa kwenye ufugaji wa samaki au watafute maeneo mengine ambayo yanafaa kwa shughuli za uzalishaji mali.

Wajumbe wa kikosi hicho walishuhudia mahindi yakiwa katikati ya vyanzo vya maji katika vijiji vya Idegenda, Madege na Kidabaga.

Hata hivyo ofisa Misitu huyo aliwekwa kitimoto na kikosi kazi “Sasa wewe hata kama wanafanya wengine wapo chini ya usimamizi wako na anayevuruga unaweza kumchukulia hatua za kisheria.”walisema wakati wakimweka kitimoto ofisa huyo

Hata hivyo hali ilikuwa ya kuridhisha katika chanzo cha mto Lukosi kwa kuwa kuna usimamizi mzuri wa viongozi wa kijiji cha Idete lakini wananchi walitaka zoezi la kuzuia vinyungu liwe la wilaya nzima.

“Tupo makini katika kutunza mazingira lakini hatujafahamu vijiji vya jirani kwamba hili linakuwaje alipoulizwa kuhusu sheria ya yoyote wanayoisimamia alisema kuwa sheria ipo na inasema kwamba mtu akichoma moto wanamtoza faini y ash.50,000 hadi 100,000.”walisema wananchi hao.

Aidha kikosi kazi hicho kilimtaka ofisa wa Misitu wilaya kusimamia sheria za mazingira na kuomba ushauri pale anapokwama ili kunusuru vyanzo vya maji.



Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.