Na Mwandishi Wetu, Mafinga. SERIKALI imerejesha kambi tano za JKT zilizokuwa zimesitishwa mafunzo ya jeshi hilo ili kuongezea uwezo zaidi wa kuchukua vijana na kuwajengea uwezo wa kuwa hodari,watiifu na waaminifu katika kambi zake. Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi wa Ustawi wa Jamii JKT Taifa Luten kanal Anchilla Kagombola kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi hilo meja jenarali Michael Isamuyo kwenye hitimisho la mafunzo ya vijana wa kujitolea (JKT) kikosi 841 KJ mafinga operation. Kambi zilizorejeshwa ni kambi 826 KJ Mpwapwa Dodoma, kambi 839 KJ Makuyuni Arusha, kambi ya 845 Itaka Songwe,846 Luha Rukwa na kambi 847 Milundokwa Rukwa na kati ya kambi hizo kambi la Makuyuni Arusha tayari wa meshaanza kuchukua vijana na wanaendelea na mafunzo. Kagombola alisema ni Imani ya Mkuu wa JKT kuwa serikali inazidi kutoa mchango wa hali na mali ili kuzidi kuboresha miundombinu ...
John Mgina maarufu kama Kichaa wa Yesu anakuja na wimbo mpya unaofanya vizuri USINIACHE YESU. Ujio wa mwaka 2017 Albam inaitwa HAYA NI MAPITO TU. Mgina anapatikana kwa namba 0756 896976.
Na Enles Mbegalo UONGOZI wa Soko la Samaki Kunduchi, Dar es Salaam limeunda Kikundi cha Ulinzi Shirikishi cha Pwani na Baharini (BMU), kwa lengo la kudhibiti uvumi haramu. Akizungumza na mwandishi wa blog hii, mmoja wa viongozi wa soko hilo, Ramadhani Ali, alisema kikundi hicho cha watu 15 kitafanya doria kwenye fukwe za bahari kwa masaa 24 ili kuwadhibiti wavuvi hao pamoja na wachafunzi wa mazingira ya fukwe hizo. “Ulinzi huu wa baharini utasaidia sana kuwaokoa baadhi ya samaki ambao wameaza kupotea kabisa baharini na tutagundua ni samaki wapi hawapatikani kwa sasa na kipindi cha nyuma walikuwa wanapatikana,”alisema Ali Pia, alisema pamoja na serikali kupiga vita uvuvi huo ila inatakiwa kuwasaidia wavuvi hao vifaa vya kisasa kwaajili ya kuvitumia katika shughuri zao za uvuvi. Hata hivyo, alisema soko hilo limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimba ikiwamo usalama mdogo kwa wavuvi kwani wamekuwa wakitishiwa maisha yao na vij...
Comments
Post a Comment