SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

 Na Mwandishi Wetu, Mafinga.

SERIKALI imerejesha kambi tano za JKT  zilizokuwa zimesitishwa mafunzo ya jeshi hilo ili kuongezea uwezo zaidi wa kuchukua vijana na kuwajengea uwezo wa kuwa hodari,watiifu na waaminifu katika kambi zake.

Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi wa Ustawi wa Jamii JKT Taifa   Luten kanal Anchilla Kagombola kwa niaba ya  Mkuu wa Jeshi hilo meja jenarali Michael Isamuyo kwenye  hitimisho la mafunzo ya vijana wa kujitolea (JKT) kikosi 841 KJ mafinga operation.  

Kambi zilizorejeshwa ni  kambi 826 KJ Mpwapwa Dodoma, kambi 839 KJ Makuyuni Arusha, kambi ya 845 Itaka Songwe,846 Luha Rukwa na kambi 847 Milundokwa Rukwa na kati ya kambi hizo kambi la Makuyuni Arusha tayari wameshaanza kuchukua vijana na wanaendelea na mafunzo.

Kagombola alisema  ni Imani ya Mkuu wa JKT kuwa serikali inazidi kutoa mchango wa hali na mali ili kuzidi kuboresha miundombinu ya vikosi vya JKT na hatimaye kuwawezesha vijana wengi wa Tanzania wenye sifa za kujiunga na mafunzo hayo kwa kujitolea na pia kuchukua vijana wengi kwa mujibu wa sheria wanaomaliza kidato cha sita.

“Ninyi vijana mnaohitimu leo hii, mafunzo haya yasitumike kupiga raia wema ninyi ni sehemu ya jamii ni watoto wa wakulima na wafanyakazi wanaohitaji ulinzi kutokana kwenu shirikianeni na mamlaka husika kuwafichua waovu wasaliti na wale wote wasiotakia Nchi yetu amani na utulivu tuliyonayo.”alisema Kagombola.

Awali akisoma risala ya wahitimu hao Diana Jason Ngaiza alisema, wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa wakufunzi wa kada ya juu, ukosefu wa vifaa vya kuendeshea mafunzo hali ambayo imepelekea mafunzo kufanyika kwa shida.
Naye Mkuu wa Kikosi hicho, Luten Kanal Hamis Mahiga alisema  kwa kipindi kifupi walichokaa kikosini hapo wameweza kuwaachia vitu mbalimbali vya maendeleo ikiwamo mashine ya kusaga na kukoboa,bwala la samaki na jenereta vitu ambavyo miaka ya nyuma vilikuwa havipo.

Mahiga alisema lengo la kuwapa nyenzo tatu kwenye kiapo chao ikiwamo uadilifu,utii na uhodari ni kuwatengezea uwezo wa kwenda kubadilisha changamoto zilizopo kwenye jamii kuwa fursa pindi wanapohitimu mafunzo yao.
Kwa upande wake mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri William alisema baadhi yao watapata nafasi ya idara mbalimbali za serikali katika utumishi wa umma huku akiwataka watumie nafasi hizo kwa kuzienzi kama tunu ili waweze kufanya kazi hizo kwa nidhamu ya hali ya juu.

Pia, William aliwaomba vijana ambao watarudi  uraiani  washiriki na wananchi wengine katika kuzalisha mali ikiwamo kilimo,ufugaji,viwanda,ujasirimali pamoja na kulinda taifa ili kuleta mapinduzi ya kiuchumi katika taifa hili.

Comments

Popular posts from this blog

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.