DIWANI URIO AZINDUA KAMPENI MPYA YA WEZESHA MAMA NA MTOTO MPYA WA KUNDUCHI IKIWA NI MOJA YA AHADI ZAKE.

  Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Diwani wa Kata ya Kunduchi, Michael Urio amezindua kampeni ya Wezesha Mama na Mtoto Mpya wa Kunduchi kwaajili ya ujenzi wa wodi ya akina mama pamoja na chumba za upasuaji katika zahanati ya Mtongani na Ununio ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Aidha Kampeni hiyo iliambatana na ufanyaji wa usafi  katika Zahanati ya Mtongani ili kuboresha mazingira ya zahanati hiyo.

Akizungumza kabla ya uzinduzi wa kampeni hiyo leo jijini Dar es Salaam, Urio alisema kampeni hiyo ni moja ya ahadi ambazo aliahidi wakati wa uchaguzi ambapo vipaumbele vyake vilikuwa sita ikiwamo  kuboreshaji mazingira ya Afya, elimu.

Vipaumbele vingine mazingira ambapo hadi sasa Kata hiyo inakitaru cha miti zaidi ya 6000, kuboresha uchumi wa wananchi, Soko la samaki la Kunduchi , sanaa na michezo na Utawala bora.

“Uzindunzi wa Kampeni hii ya Wezesha Mama na Mtoto Mpya wa Kunduchi ni moja ya utekelezaji wa  ahadi ambazo niliahidi wakati wa uchaguzi ,”alisema

Diwani Urio alisema uzinduzi wa kampeni hiyo utaendana na  uboreshaji wa viwanja vya wazi vya mipira,  Mashindano ya mpira Urio Cup, upandaji wa miti,   riadha pamoja  Msonge Mara Soni ambayo itazinduliwa siku za karibuni.

 Aliwaomba wadau mbalimbali kuunga mkono jitihada hizo kwa kuchangia ili aweze kutekeleza ujenzi  wa chumba cha upasuaji katika zahanati ya Mtongani na Ununio.

“Kupitia Kampeni hii nitahakikisha nasimamia vizuri na wadau wa makampuni, Taasisi za kifedha tunaomba mtupokee vizuri tutakapo kuja kwaajili ya kuwaomba  ili tuweze kufikia lengo la kupata sh. milioni 300 kwaajili ya kufikia lengo letu,”alisema

Alisema kupitia Halimashauri ya Manispaa ya Kinondoni wameweza kupatiwa zaidi ya sh.milioni 3 kwaajili ya kuboresha Zahanati ya Tegeta, sh. milioni 100 kwaajili ya kuboresha Soko la Tegeta Nyuki na sh. milioni 150 kwaajili ya kuboresha soko la samaki Kunduchi.

Naye, Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Festo Dugange alisema  lengo la Serikali  kuboresha ni kuboresha huduma ya mama mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano ili kupunguza idadi ya vifo ambavyo vimekuwa vikitokea.

Katika uzinduzi wa Kampeni hiyo wananchi na wageni waalikwa waliohudhuria wamechangia zaidi ya sh. Milioni 4 na mifuko ya saruji 50.
 Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Kinondoni Kazi Maduhu, kulia  akimpongeza Diwani Urio kwa kuzindua Kampeni hiyo itakayosaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto.

 Diwani wa Viti Maalum Manispaa ya Kinondoni ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake  UWT Kinondoni, Florence Masunga, kulia  akitoa ahadi yake ya kuchangia sh. 500,000 ili kuunga mkono juhudi za kampeni hiyo, kushoto ni Diwani Urio.

 
 Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Festo Dugange, kulia  akizungumzia juu ya jitihada za Serikali za kukabiliana na vifo vya mama na mtoto na ameahidi kuchangia mifuko ya sumenti 15 kwaajili ya Kampeni hiyo kushoto ni Diwani Urio.

 Diwani Urio, kushoto akiwa kwenye mazungumzo na baadhi ya wageni waalikwa kabla ya uzinduzi wa Kampeni hiyo leo jijini Dar es Salaam, katikati ni  Meja Msaki kutoka chuo cha NDC,na kulia ni Luteni Baraka Myala kutoka Kunduchi Transt  Camp (KTC).

 Diwani Urio, kushoto akiwa na picha ya pamoja na wageni waliohudhuria uzinduzi huo, wa kwanza kulia ni Diwani wa Kata ya Mabwe Pande  Suzan Massawe.


Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Kilongawima Kata ya Kunduchi,John Rugakila akitoa ahadi ya kuchangia mifuko 10 ya sumenti baada ya kukaribishwa na mwenyeji wake Diwani Urio katika uzinduzi wa Kampeni hiyo leo.

 Diwani Urio akikabishia fedha taslimu sh. 200,000 kutoka kwa Meja Margreth Msaki kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDS)  kwaajili ya kuchangia juhudi za uzinduzi wa Kampeni hiyo leo, iliyofanyika katika Zahanati ya Mtongani.

 Diwani Urio kushoto  akizungumza na Mwenyekiti wa Joggingi zote Kata ya Kunduchi, Hamisi Yusuph, kulia.

 Diwani wa Kata ya Kunduchi Michael Urio akiwa na Mjumbe wa Kipindupindu Taifa Melone Afrika ambaye alizungumza kwa niaba ya wenzake.

 Wageni waalikwa wakiwa katika picha ya pamoja  leo baada ya uzinduzi wa Kampeni hiyo na Diwani Urio, wa tatu kutoka kushoto, na wa pili kutoka kushoto ni Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni Festo Dugange na kulia kwa Diwani Urio ni Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Kinondoni Kazi Maduhu.

PICHA ZOTE NA MAISHA NI HABARI BLOG

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.