MAJAMBAZI WAVAMIA MGODI NA KUPORA SH. MILIONI 80.


Na Mwandishi Wetu, Iringa

KUNDI la watu wanaosadikika kuwa ni majambazi wamevamia mgodi wa machimbo ya dhahabu wa  Nyakavangala iliyopo kwenye tarafa ya Isimani Wilaya ya Iringa  na kuiba fedha zaidi ya sh.Mil.80.

Aidha watu hao wamefanikiwa kuiba dhahabu zenye uzito wa gramu 490 na simu nne za mkononi za wafanyabiashara  na kujeruhi watu tisa.

 Taarifa hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, alisema majeruhi hao wamepelekeka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa  kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Kasesela alisema alipokea simu kutoka kwa wananchi waliopo kwenye mgodi huo ambao walimueleza kwamba kuna milio ya bunduki lakini  aliwasiliana na  jeshi la polisi na jeshi hilo lilienda eneo la tukio kwa kuchelewa kutokana na jiografia ya eneo ilivyo na kukuta majambazi hao wametokomea kusikojulikana.

 Alisema  majambazi hao walikuwa na silaha za moto pamoja na silaha za jadi.
 Pia Kasesela aliwataja majeruhi hao ambao ni Mginya Paulo Gadae(38) mkazi wa Morogoro ambaye wamemvunja mkono na migu,  Bakari maarufu kwa jina la mzee (Beka) na kusema kuwa mzee huyu wakati anatoka machimboni alikutana na majambazi hao ambao walimpiga vibaya na hadi sasa yupo kwenye chumba cha uangalizi maalumu cha wagonjwa mahututi na Sungari Shija (24)mkazi wa geita ambaye aliumizwa miguu.
 Majeruhi wengine ni Fadhili Naringa Ramadhani mkazi wa Kingonguila Morogoro,Msulwa Msanga (30) mkazi wa Bariadi , Odrick Michael(33) mkazi wa Iringa Ipogolo, Kitandu Magula (27) mkazi wa tanga,Daniel masonja(40) mkazi wa Simiyu na Eliya Mushi ambaye anatoka mkoa wa Kilimanjaro Moshi.
Kasesela  aliwataka wananchi hasa wanaoenda eneo hilo kuacha kutembea na fedha nyingi na badala yake watumie benki.
 “Eneo hilo halina mitandao ya simu na hata wakiotupigia simu walitumia njia mbadala kwa kutoka nje ya eneo hilo,” alisema Kasesela na kuongeza .
“Watu hao walitokomea kusikojulikana kwani  kule hakuna njia nyinyine ya kutokea na kuingilia na jeshi hadi sasa linaendelea na msako kuhakikisha linawakamata majambazi hao,”
Alisema kuwa kwa sasa waliopo mgodini wameanza na shughuli ya utambuzi na kuongeza kuwa majambazi hao wakati wanavamia na kuumiza walikuwa wanawaambia tuoneshe mtu fulani.
  “Hawa watu walienda kwa tageti kubwa sana kwa sababu wakati wameingia kwenye mgodi huo walikuwa wanawaambia tuoneshe mtu fulani.”alisema Kasesela.


Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.