VIONGOZI WA DINI YA KIISILAMU WAOMBWA KUTOTOA HIFADHI KWENYE NYUMBA ZA IBADA.

Na Mwandishi Wetu, Kilolo.

SERIKALI mkoani Iringa imewaomba   viongozi wa dini ya kiislamu kutowaruhusu watu wasiowafahamu  kuwapa hifadhi kwenye nyumba zao za ibada na badala yake wawape hifadhi watu wanaowafahamu ili kutowapa nafasi wanaoitumia dini hiyo kwa uovu.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu  wa Mkoa wa Iringa,  Amina Masenza wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa serikali,madhehebu ya dini kutoka kona zote za mkoa wa Iringa na wananchi wengine ambao walijumuika kwa pamoja kwenye hafla ya chakula cha jioni (futari) kilichoandaliwa na halmashauri ya wilaya ya Kilolo mkoani Iringa.

Masenza  alisema kuna baadhi ya maeneo  kumeibuka tabia ya watu kutumia kigezo cha dini kufanya vitendo viovu ikiwamo utapeli na uasi jambo linalolenga kuchafua dini ya uislamu.

“Niwaombe viongozi wangu wa dini msitumie kipindi hiki cha mfungo kuwaruhusu watu msiowafahamu kulala kwenye nyumba za ibada kwa sababu kuna watu wanatumia mgongo wa misikiti kufanya maovu na kuchafua dini yetu.”alisema Masenza

Katika hatua nyingine mkuu huyo alitumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wananchi kuunga mkono serikali ya awamu ya tano kwa kuwa inawaletea maendeleo ya kweli kwenye maeneo yao.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilolo  Asiah Abdallah na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jumuhuri Willium walisema  licha ya kuwataka wananchi na waumini wa dini ya Kiislamu kutumia vyema mwezi huo mtukufu wa ramadhani  jamii ijikite katika kuombea kazi nzuri  zinayofanywa na Rais Dk.John Magufuli.


Kwa upande wao shekhe wa Mkoa wa Iringa, Abubakari Chalamila na wa Wilaya ya Kilolo Athuman Mnyambwa walisema  mapambano aliyoyaanza rais yanalenga kutetea rasilimali za taifa pamoja na kuwatetea  wananchi wanyonge.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.