MIKOA YA IRINGA NA NJOMBE WATOTO WANAPATWA NA UTAPIAMLO NA KUDUMAA KWA KUKOSA LISHE.

Na Mwandishi Wetu, Iringa.

IMEELEZWA kwamba watoto wengi nchini wanapatwa na tatizo la utapiamlo pamoja na kudumaa kwa sababu ya kukosa lishe bora kutokana na wazazi kutokuwa na uelewa kuhusu lishe bora kwenye familia zao.

Aidha Mikoa ya Iringa na Njombe ni mikoa inayolima mazao ya chakula kwa wingi ikiwamo viazi, uwele, ngao pamoja viazi vitamu lakini licha ya kuwa na sifa hizo za uzalishaji bado wazazi hawana elimu ya kuwapatia watoto wao lishe bora. 

Wito huo umetolewa na Umoja wa Wanafunzi wa Chuo Kikuu Kikatoliki cha (RUCU), wanaosomea sayansi ya afya na mazingira (REHSA).

Wakizungumza na wazazi na walezi  jana kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa baadhi ya wanafunzi wa Chuo hicho Wajabu Abdulrahaman na Fadhili Katula walisema kuwa wao kama wanafunzi wameandaa mafunzo kwa lengo la kutoa elimu ya lishe kwa kina mama wanaolea na wajawazito.

 Hata hivyo walisema mafunzo hayo yatalenga pia  wazazi wenye watoto waliochini ya umri wa miaka mitano ili waweze kupambana na tatizo la udumavu na maradhi.

Wanafunzi hao walisema baada ya kutoa elimu hiyo, wanatarajia kuona jamii ya Iringa ikizingatia lishe bora huku wakizungumzia changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo wakati wa utoaji elimu hiyo kwa jamii. 

Walisema  moja ya changamoto wanazokumbana nazo ni uelewa mdogo kutoka kwenye jamii juu ya lishe bora, hawajui ni vyakula gani vinapatikana kwenye maeneo yao ambayo yanawasaidia akina mama wajawazito pamoja na watoto wao. 


 Ofisa Lishe Hospitali ya Mkoa wa Iringa, Neema Mtekwa , alisema muitikio wa jamii juu ya lishe ni hafifu hususani kwa kina baba hali iliyosababisha kushindwa kufikia lengo la kutokomeza udumavu kwa watoto. 


REHSA ni umoja wa wanafunzi wanaosoma Sayansi ya Afya na Mazingira katika Chuo Kikuu cha Rucu ambao wamekuwa wakizunguka katika kata mbalimbali za Mkoa huo kwa lengo la kutoa  elimu kwa jamii ili kuondokana na tatizo la udumavu na utapiamlo kwa watoto mkoani Iringa. 





Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.