Zefrin Lubuva, afungua blog ya mtaa, S MTAA OYSTERBAY.BLOGSPOT.COM

Na Enles Mbegalo

MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa Oysterbay, Zefrin Lubuva, amefungua blog ya mtaa wake kwaajili ya kutumia mambo mbalimbali ya kimaendeleo kwenye mtaa wake.

Akizungumza na mwandishi wa blog hii jijini Dar es Salaam leo, Lubuva, alisema ufunguzi wa blog hiyo ni moja ya ahadi zake ambazo alizitoa  kwa wakazi hao wakati wa uchaguzi.

“Mtaa wangu ulikuwa hauna blog na nimetekeleza hili ili liweze kutusaidia kwaajili ya kupeana taarifa  mbalimbali za maendeleo zinazofanyika kwenye mtaa wetu,”alisema Lubuva

Lubuva, alisema wadau mbalimbali walio kwenye mtaa wetu wamekuwa wakichangia huduma mbalimbali kwaajili ya maendeleo ya  mtaa na blog hii itasaidia wananchi kuwafahamu wadau hao zaidi na huduma ambazo wamekuwa wakizitoa kwenye mtaa.

“Blog yetu ya mtaa wa Oysterbay nataka iwe ya mfano katika mitaa yote ya Dar es Salaam,”alisema




Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.