WATU WA NANE WAVAMIA MKUTANO WA CUF NA KUJERUHI.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

BAADHI ya waandishi wa habari na wanachama wa Cufu wajeruhiwa baada ya watu wanane, waliokuwa wamevalia ninja na kuvamia mkutano wa wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), mabibo jijini Dar es Salaam.

Vurugu  hizo zimetokea leo, wakati  wanachama wa CUF walipokuwa kwenye mkutano huo na waandishi wa habari katika Hoteli ya Viva jijini Dar Es Salaam.

Vurugi hizo zilizua taharuki kubwa kwa waandishi wa habari na wakazi wa eneo hilo ambapo walifanikiwa kumkamata mmoja wa watuhumiwa hao na kumkata mguu wa upande wa kulia.

Hata hivyo baadhi ya mashuhuda wanasema watu wasiojulikana walifika katika eneo hilo wakiwa wamefunika nyuso zao na vitambaa huku wakitumia silaha za jadi.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Suzan Kaganda, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na taarifa zaidi atatujuza baada ya kufika eneo la tukio.

Mmoja wa watuhumiwa akipambana na wananchi baada ya kukamatwa eneo la tukio jijini Dar es Salaam. 
Mmoja wa watuhumiwa waliovamia mkutano huo akiwa chini ya ulinzi baada ya kukatwa mguu wake wa kulia na wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.