DIWANI URIO AWA MIONGONI MWA WALEZI WA KITUO CHA WATOTO YATIMA AMANI ORPHANAGE.

 Na Enles Mbegalo

DIWANI wa Kata ya Kunduchi jijini Dar es Salaam, Michael Urio,amejitolea kuwa miongoni mwa wazazi watakao kuwa walezi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Amani Orphanage, kilichopo Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Aidha, Diwani Urio  alijitolea wakati  alipokuwa mgeni rasmi katika uchangishaji wa harambee kwaajili ya kuchangisha fedha za kusaidia katika kutatua baadhi ya changamoto zilizopo kwenye kituo hicho.

“Na mimi nitakuwa miongoni mwa wazazi watakao lea kituo hiki na shida yangu itakuwa shida yao, kama nilivyo mzazi wa familia yangu naomba niwe mzazi wa kituo hiki,”alisema Urio na kuongeza kuwa

“Mkurugenzi usisite kunishirikisha kitu chochote iwe chakula, mavazi, malazi nitawasaidia kwa nilichonacho na nitawasaidia kuomba kwa wadau mbalimbali kwaajili ya watoto hawa,”

Hata hivyo pamoja na ulezi huo Diwani Urio aliahidi kutoa Sh. Milioni moja pamoja kusaidia kufikisha umeme kwenye eneo hilo kutokana na kutokuwa na umeme.

Pia Diwani Urio ameahidi kusaidia ujenzi wa madarasa ya Shule kwenye eneo la kituo hicho kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Kituo hicho alimshukuru Diwani Urio kwa kuweza kuchangisha zaidi ya Sh. Milioni Sita kwenye harambee hiyo ambazo zitatumika katika kuweka Solar kwenye eneo hilo na kutatua baadhi ya changamoto za kwenye kituo hicho.
 Diwani  Urio akiwa Pamoja na  Mkurgenzi wa Kituo hicho akimpeleka sehemu ya kukaa mara baada ya kufika kwenye kituo hicho.

 Diwani Urio akipiga makofu wakati wa uchangishaji wa harambee hiyo  katika kituo hicho leo.

 Diwani Urio aliyenyanyua mtoto akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wadau na watoto wanaolelewa kituo hicho .

 Mkurugenzi wa Kituo hicho  pamoja na Diwani Urio wakicheza wakati mwimbaji wa Nyimbo za Injili, Christina Mbilinyi akitumbuiza kwenye hafla hiyo iliyofanyika kwenye kituo hicho.

 Baadhi ya wada wa kituo hicho kutoa TEAMTEZZA na TEAMVW zinazohusika na ushindanishaji wa mbio za magari, kutoka Kunduchi jijini Dar es Salaam.

 Melone Africa katika akiwa na baadhi ya watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho.

 Baadhi ya wadau wakiwa wanaondoka kwenye kituo hicho baada ya hafla hiyo kumalizika.

 Miongoni mwa wadau walioshiriki kwenye hafla hiyo leo wakiwa kwenye picha ya pamoja.

PICHA ZOTE NA MAISHA NI HABARI BLOG.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.