MAKINDA KUFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA KUJADILI MAENDELEO YA TANZANIA NA KOREA KESHO.


Na Mwandishi Wetu.

SPIKA  wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mstaafu Anne Makinda,  anatarajiwa kufungua mkutano  wa wadau mbalimbali wa kujadili maendeleo ya Tanzania na Korea Kusini na nchi nyingine za Asia kesho jijini Dar es Salaam.

Aidha mkutano huo wa siku tatu utafanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Budget Entertainmemt Resort uliopo karibu na Hotel ya Bahari Beach.

Akizungumza na mwandishi wa blog hii, Rais na Mwazirishi wa Taasisi  hiyo  isiyokuwa ya Kiserikali ya Chingu Kota Centre, Andrew Dyson Bukuku alisema mkutano huo utajadili maendeleo mbalimbali  ikiwamo kwa nini Korea Kusini imepiga hatua kiuchumi.

Bukuku alitolea   mfano wa miaka ya 1970 na 1980 ya nchi ya Korea ilikuwa tofauti kiuchumi  na sasa na nchi hiyo imeweza kupiga hatua kwa maendeleo.

Alisema kuwa  miaka hiyo Korea Kusini uchumi wake ulikuwa sawa sawa na nchi za Afrika lakini leo hii nchi hiyo ni moja kati ya nchi zenye uchumi mkubwa dunia.

“Kazi ya Taasisi ya Chingu Kota Centre ni kuandaa matamasha ambayo yanahusu Korea pamoja na nchi zingine za Asia kwa ujumla na katika hayo matamasha yatahusu kujadili  maendeleo kwa mfano miaka ya 1970 hadi 1980 Korea Kusini uchumi wake ulikuwa sawa sawa na nchi zenye uchumi mkubwa duniani,”alisema

Bukuku aliongeza kuwa Chingu Kota Centre pia husimamia matamasha ya watu kujifunza maendeleo au mambo mbalimbali ya Kikorea na ni kama daraja la mahusiano kati ya Korea na Tanzania katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya Tano ya Rais John Pombe Magufuli kwa kufungua Ubalozi wa Tanzania nchini Korea Kusini.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.