NBS IMEANZA MAANDALIZI YA UTAFITI WA MATUMIZI YA TUMBAKU KWA WATU WAZIMA NCHINI.

 Mtaalam wa Utafiti wa Matumizi ya Tumbaku kwa Watu wazima, David Plotner (kushoto) kutoka shirika la CDC Marekani akijadiliana na maafisa wa TEHAMA wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Munir Mdee (katikati) na Abdullah Othman (kulia) wakati wa mafunzo ya awali ya utafiti huo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Utafiti wa Matumizi ya Tumbaku kwa Watu wazima unatarajia kufanyika nchini mwezi Agosti, 2017.

 Afisa TEHAMA kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Munir Mdee akitoa mafunzo ya kutumia Dodoso kwa njia ya tablet kwa washiriki wa mafunzo ya Utafiti wa Matumizi ya Tumbaku kwa Watu wazima wakati wa mafunzo ya awali ya utafiti huo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

 Mratibu wa  Utafiti wa Matumizi ya Tumbaku kwa Watu wazima,Hellen Hillary (kushoto) kwa upande wa Tanzania Bara akijadiliana na mratibu wa utafiti huo kwa upande wa Tanzania Zanziar , Nuru  Masoud (kulia) wakati wa mafunzo ya awali ya utafiti huo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. 

 Meneja wa Takwimu za Jamii, Sylvia Meku (katikati) akiwaelekeza washiriki wa mafunzo ya awali ya Utafiti wa Matumizi ya Tumbaku kwa Watu wazima, Frank Mapendo (kushoto) na Jocelyne Rwehumbiza (kulia) wakati wa mafunzo ya awali ya utafiti huo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

 Mwananchi kutoka kata ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam akijibu maswali kutoka kwa Mtakwimu, Stephen  Cosmas wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu wakati wa majaribio ya Dodoso litakalotumika wakati wa Utafiti wa Matumizi ya Tumbaku kwa Watu wazima unaotarajia kufanyika nchini mwezi Agosti, 2017.

Mtakwimu Hellen Mtove wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu akimhoji mwananchi kutoka kata ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam wakati wa majaribio ya Dodoso litakalotumika wakati wa Utafiti wa Matumizi ya Tumbaku kwa Watu wazima unaotarajia kufanyika nchini mwezi Agosti, 2017.

(PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO)]

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.