NBS, MFUMUKO WA BEI WA MWEZI HUU HAUJAONGEZEKA.

Na Enles Mbegalo

MFUMUKO wa bei wa Taifa wa mwezi Aprili 2017  umebakia kuwa asilimia 6.4 kama ilivyokuwa mwezi Machi 2017.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii na Sensa ya Watu na Makazi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo, alisema  inamaanisha  kasi ya upandaji  ilivyokuwa kwa mwaka ulioisha mwezi Machi 2017 imekuwa sawa.

Pia alisema fahirisi za bei zimeongezeka hadi 109.4 mwezi Aprili 2017 kutoka 102.46 mwezi Aprili 2017.

Kwesigabo aliongeza kuwa,mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula nyumbani na migahawani kwa mwezi Aprili 2017 umeongezeka hadi asilimia 11.8 kutoka asilimia 11.0 ilivyokuwa mwezi Marchi 2017.

 “Mfumuko wa bei wa Taifa wa mwezi Aprili 2017 umebakia kuwa asilimia 6.4 kama ilivyokuwa mwezi uliopita  na  hii inamaanisha kuwa, kasi ya upandaji wa bei za bidhaa za mwezi huu na mwezi ulioisha zilikuwa sawa,”alisema Kwesigabo

Alifafanua kuwa,mfumuko wa bei wa mwezi Aprili 2017 unaopimwa kwa mwezi umeongezeka kwa asilimia 0.5 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 1.4 ilivyokuwa mwezi Machi 2017.

“Fahirisi za bei zimeongezeka hadi 109.04 mwezi Aprili 2017 kutoka 108.44 mwezi Machi 2017 kuongezeka kwa fahirisi hizo kumechangia kuongezeka kwa bei za baadhi ya vyakula,”alisema

Alisema baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa fahirisi ni pamoja na mahindi kwa asilimia 4.8, unga wa mahindi kwa asilimia 7.1, choroko kwa asilimia 6.5, viazi mviringo kwa asilimia 4.0, nyanya kwa asilimia 7.8, nazi 6.9, mihogo 5.9 na vitunguu 3.5.

Akizungumzia thamani ya shilingi ya Tanzania  alisema uwezo wa sh.100 katika kununua bidhaa na huduma umefikia sh.91 na senti 71 mwezi Aprili 2017 ikilinganishwa na sh. 92 na seti 21 kwa mwezi Machi mwaka huu.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi za Takwimu jijini Dar es Salaam leo.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.