MSAMBATAVANGU AACHIWA BAADA YA KUSOTA RUMANDE KWA SIKU SITA.


Na Mwandishi Wetu, Iringa.

SIKU   sita za aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa,  Jesca Msambatavangu kuonja kaa la moto baada ya jeshi la polisi mkoani hapa kumshikilia na kusota rumande  pasipo kupewa dhamana .

Hata hivyo baada ya kusota kituoni hapo hatimaye  Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa imemuachia aliyekuwa mwenyekiti huyo   baada ya kukana shitaka linalomkabili.

Akisoma shauri hilo wakili wa serikali  Alex Mwita alisema mshitakiwa anashtakiwa kwa kosa la kumshambulia Neema Nyongole Februari 17 mwaka huu eneo la Kibwabwa m Manispaa ya Iringa  kinyume na kifungu cha sheria namba 240 cha mwaka 2002.

 Mwita alisema kuwa shauri hilo limefikishwa Mahakamani hapo kwa mara ya kwanza ili mshitaiwa aweze kujua shitaka lake na mara baada ya kusomewa shitaka hilo mshitakiwa  alikana kutenda kosa hilo .

Wakili Mwita alisema kuwa upelelezi wa shitaka hilo bado unaendelea huku upande wa utetezi ambao unaongozwa na mawakili wawili ambao Alfred Mwakingwe akisaidia na Jackson Chaula waliiomba Mahakama hiyo kumuachia kwa dhamana   kwa sababu kosa linalomkabili mtuhumiwa linaruhusu kupewa dhamana. 

 “Tunaomba mahakama yako tukufu impe dhamana mshtakiwa kwa sababu kosa lake linaruhusu kupewa dhamana kwa kuzingatia vigezo na mashariti”alisema Mwakingwe

Kwa upande wake hakimu mkazi mfawidhi wa mkoa wa Iringa  David Ngunyale alisema kuwa mshitakiwa anaweza kudhaminiwa na watu wawili ambao wanakidhi vigezo vinavyowekwa na mahakama  kwa kuweka bondi ya tsh Mil moja kwa kila mmoja pamoja na mali isiyoamishika.


 Hata hivyo mshitakiwa aliweza kuleta wadhamini wawili ambao ni Anna Mchami na Frank Andrea wote wakazi wa mkimbizi  Manispaa ya Iringa wakiwa na baerua ya utambulisho pamoja na hati za nyumba. 

 Hakimu Ngunyale alisema kuwa kwa kuwa mshitakiwa ameleta wadhamini wawili ambao wamesaini vilelelezo hivyo mahakama imeamuru kumuachia huru na shauri hilo litatajwa tena Juni 1 mwaka huu.

Hivi karibuni mwenyekiti huyo alifukuzwa uanachama akiwa ni miongoni mwa makada wa CCM ambao walifukuzwa uanachama na rais Dk.John Pombe Magufuli mjini Dodoma.

Wengine waliofukuzwa ni aliyekuwa mwenyekiti wa jumuiya ya wanawake wa CCM (UWT)  Sophia Simba na aliyekuwa mwenyekiti wa chama  hicho mkoa wa Dar Es salaam Ramadhani Madibida pamoja na wenyeviti wa mikoa mingine.



Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.