TIRA YASHAURIWA KUPELEKA ELIMU YA BIMA KWA MADAKTARI.

Na Mwandishi Wetu, Mafinga.

MAMLAKA ya Kusimamia Shughuli za Bima Nchini (TIRA) imeshauriwa kupeleka elimu ya bima kwa madaktari walio kazini ili kuhakikisha watanzania wanaopata ajali kwenye vyombo vya moto wanalipwa fidia na makampuni ya bima.

Aidha hiyo ni  kinyume na sasa ambapo waathirika wengi wa ajali za moto hawafaidiki na malipo ya bima kutokana na kukosa uelewa.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Maofisa Tabibu cha Mafinga (COTC), Israel Mwakasonda wakati  Mamlaka ya TIRA walipotoa elimu ya bima kwa wanafunzi wa chuo hicho mjini hapa.

Alisema  serikali pia inapaswa kuwatazama madaktari na kuwakatia bima kutokana na hatari nyingi wanazokumbana nazo wakiwa kazini.

 Mwakasonda alisema kuwa “hili ni nalo ni suala la kuwafikiria na kuwaelimisha ili wapate bima kwa ajili ya kazi zao kwa sababu kazi za udaktari kwa wakati mwingine zina madhara yake,” alisema  Mwakasonda na kuongeza

“Unaweza ukajiumiza wakati unahudumia mgonjwa,wagonjwa wengine wanamatatizo ya akili na mengine mengi na unaweza kupata madhara wakati unamtibu huyo mgonjwa wa akili na ugonjwa huo ukaambukizwa hata wewe daktari.”

 Naye, Meneja wa TIRA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Hilard Maskini, alisema Mamlaka hiyo inaendelea kutoa elimu ya bima kwa makundi mbalimbali lengo likiwa ni kuhakikisha kila mtanzania anakuwa na uelewa wa uwapo wa bima na kufaidika na mafao ya bima mara wanapopata majanga.

 Mwakilishi wa Makampuni ya Bima Nyanda za Juu Kusini, Julius Mayamba, akiwataka abiria kutopanda magari yaliyojaza kupita kiasi.

Maskini alisema  kwa kuanzia wameamua kuanzia na Maofisa Tabibu ambao ni wanafunzi kwa sababu mara nyingi kwenye fani hizo wanakutana na watu wengi.


Alisema  mfano watu waliopata ajali lakini kuhusu kutoa elimu kwa madaktari ambao wapo kwenye hospitali ambao ndio wanakutana na watu ambao wamepata ajali watakuwa wanawapa elimu hiyo na kuwa endelevu pamoja na kutoa elimu hiyo kwenye hospitali mbalimbali nchini.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.