MANISPAA YAOMBWA KUSIMAMIA FEDHA ZINAZOTOLEWA KWA WATENDAJI WA MITAA.

 Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Sea View, Kata ya Kivukoni, Manispaa ya Ilala, Victor Muneni ameiomba Manispaa hiyo  kusimamia fedha zinazotolewa kwa  watendaji wa Mitaa  kwaajili ya shughuli mbalimbali za mitaa kwani fedha  hizo zimekuwa hazifiki kwenye mitaa hiyo.

Aidha, kitendo hicho kimekuwa kikichangia  migogoro kwenye ofisi za mitaa na kuongeza wimbi la rushwa kwa wananchi wanaohudumiwa katika ofisi hizo kwani watendaji hawanunui vifaa kwaajili ya matumizi ya ofisi.

Akizungumza na mwandishi wa blog hii, Muneni alisema watendaji hao wamekuwa wagumu kutoa fedha hizo, zinazotolewa na  Manispaa kwaajili ya matumizi ya stationary kwa kutotoa fedha hizo zimekuwa zikichochea upokeaji wa rushwa kwa Wenyeviti wa mitaa kwa fedha hizo zimekuwa hazifiki kwao.

Alisema Wenyeviti hawana jinsi ya kupata fedha nyingine kwaajili ya kutolea huduma hiyo ya Stationary ni jukumu la Manispaa.

Aliongeza kuwa Manispaa  husambaza fedha hizo kwenye kata zote kwa matumizi ya kununua stationary za Ofisi za Mitaa yake lakini watendaji hawatekelezi maagizo hayo na fedha hizo Manispaa huzitoa kwa maelekezo na matumizi yake.

Alisema kutokana na fedha hizo  kutofika kwenye ofisi hizo inawawia vigumu kutoa huduma bora  na hiyo inachangia wenyeviti kuwatoza fedha  wananchi wakati wanapohitaji kuhudumiwa katika ofisi hizo.

“Naiomba Manispaa isimamie watendaji wa mitaa kwani wamekuwa moja ya chanzo cha migogoro kwenye ofisi zetu za mitaa kutokana na kutofikisha fedha hizi,”alisema Muneni na kuongeza.

“Fedha nyingine zinazokuja kwenye uhamasishaji kwenye baadhi ya mambo ikiwamo  Afya haziwafikii walengwa na badala yake zinaliwa na wanaokabidhiwa,”
Hata hivyo alilalamikia kitendo cha Maafisa Afya kutotembelea mitaa na kukagua hali ya mazingira kwenye mitaa na badala yake wamekuwa wakitembelea  maeneo ya biashara tu.

“Maafisa Afya hawasimamii shughuri zao kwenye mitaa na wanatokea  baada ya muda mrefu  na wanapotokea kwa kipindi hicho huwapa adhabu  kali kwa kuwapiga faini wananchi badala ya kutoa elimu juu ya afya ya mazingira kwani wananchi wengi hawana uelewa na sheria ndogo ndogo za Manispaa,”alisema

Aliongeza kuwa maafisa hao wanatakiwa kupita kila wakati kwenye mitaa kwaajili ya kukagua mazingira  na kutoa elimu kwa wananchi hivyo wao hawafanyi hivyo.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.