WATUMISHI 134 WAKUTWA NA VYETI VYA KUGUSHI HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI.


Enles Mbegalo

WATUMISHI 134 wakutwa na vyeti vya kugushi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MHN) jijini Dar es Salaam.

Aidha, watumishi hao ni kutoka zaidi ya idara 10 ikiwamo idara ya upasuaji.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwenye vyombo vya habari leo, kutoka kwa Mkurugenzi  Mtendaji wa MHN, Profesa Lawrence Museru,  inasema wafanyakazi hao wamebainika kuwa na vyeti vya Sekondari vya kugushi.

Taarifa hiyo inasema kuwa, watumishi hao ni kutoka idara ya Kurugenzi ya Uuguzi watumishi 70,  Kurugenzi ya Tiba watumishi 20, Kurugenzi ya Tiba Shirikishi watumishi 14,  Kurugenzi ya Upasuaji watumishi wanne,  Kurugenzi ya Tehama watumishi 11.
Idara nyingine ni Kurugenzi ya Rasilimali watu, watumishi wawili,  Kurugenzi ya Ufundi watumishi watatu,  Kurugenzi ya Fedha na Mipango  watumishi watatu,  JKCI Staff in MNH vote watumishi watatu, Taasisi ya Sayansi Shirikishi za Afya  mtumishi mmoja na Vitengo vinavyoripotiwa kwa Mkurugenzi Mtendaji watumishi watatu.

Pia taarifa hiyo imesema endapo mtu hatoridhika na uamuzi huo kuhusiana na uhalali wa vyeti vyao wametakiwa kukata rufaa kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kabla ya tarehe 15 mei mwaka huu, na barua zipitie kwa Mkurugenzi Mtendaji wa MHN.

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.