BARAZA LA MADIWANI LAUTAKA UONGOZI WA WILAYA IRINGA KUTEKETEZA ZANA ZA UVUVI HARAMU.


 Na Mwandishi Wetu. Iringa.

BAADHI ya Madiwani wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Iringa vijijini, limeutaka uongozi wa Wilaya ya Iringa kuteketeza zana haramu za uvuvi zilizokamatwa kwenye msako wa kukamata zana haramu za uvuvi katika bwawa la Mtera kwakuwa zana hizo zimegeuzwa biashara na baadhi ya watendaji ambao wanaohifadhi zana hizo.

Madiwani hao waliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye  kikao cha baraza hilo ambapo baadhi ya madiwani wamehoji uhalali wa samaki wadogo kuendelea kuuzwa katika baadhi ya masoko mkoani hapa likiwamo soko kuu la mjini Iringa huku mamlaka zinazohusika zikiendelea kulifumbia macho jambo hilo.

Nao baadhi ya madiwani wa halmashauri hiyo akiwamo Diwani wa Kata ya Migori,  Majaliwa Lyaki alisema kuwa”Kuna watu wanapiga dili na kuna siku moja nilikuwa nashuhudia kati ya wale waliopo kwenye kikosi kazi amesema aliitangaziwa donge nono la sh.300,000 ili kokora lake lipate kuondoka ni kwasababu tu nyavu zimekaa muda mrefu pale,na mara nyingi tumekuwa tukifanya mawasiliano na wataalamu hakuna lolote zaidi ya kusema tu kwamba Mkuu wa Wilaya atakuja kuyachoma na hatujui anakuja kuchoma lini.”alisema Lyaki.

Diwani wa Kata ya Lowa, Charles Nyagawa, alitaka kujua kwa mfano mtu akikamatwa na pembe za ndovu zikisafirishwa kwenda Dar es salaam hawasemi mamlaka tofauti wanamkata sasa leo samaki wadogo wanauzwa sokoni na kutaka kujua hilo suala la samaki ni suala la kitaifa au nisuala la halmashauri?
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Iringa, Abel Mgimwa, alisema Halmashauri yake itazingatia ushauri wa Baraza la Madiwani kukomesha uuzwaji wa samaki wachanga hasa katika soko kuu la mjini Iringa ili kuhakikisha wavuvi na wafanyabiashara wanapenya na kutorosha samaki hao wachanga wanadhibitiwa hadi sokoni.

“Sisi kama Halmashauri tutawasiliana na mamlaka stahiki za hilo soko mamlaka zote zinazohusika na hilo soko kuwahakikishia kwamba hawatakiwi kuuza hao samaki wadogo pale hivyo ushauri tumeupokea tukishakutana nao tutawaeleza na wao waeleze kuchukua hatua stahiki dhidi ya samaki hao.”alisema Mgimwa.

Halmashauri ya Iringa Vijijini kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Iringa imekuwa ikiendesha msako wa kukamata zana haramu za uvuvi pamoja na samaki wachanga wanaovuliwa kinyume cha sheria.


 Hata hivyo  zoezi hilo limeonesha kutofanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na baadhi ya Halmashauri zinasimamia baadhi ya maeneo ya bwawa la Mtera ikiwamo Mpwawa na Chamwino  kushindwa kuendesha zoezi kama hilo .

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.