MAKINDA NIDHAMU YA KAZI NA KUJALI MUDA NDIO KILICHOWAFANYA KOREA KUSINI KUFANIKIWA.

Na Mwandishi Wetu.

SPIKA wa Bunge wa Jamhuri ya Muungo wa Tanzania Mstaafu, Anne Makinda, amesema nidhamu ya kazi na kujali muda ndio kilichowafanya Korea Kusini kufanikiwa kimaendeleo.

Hayo aliyasema jana, wakati akizindua Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ya Chingu Kota Centre inayojishughurisha na kutangaza utamaduni wa Korea nchini Tanzania.

Makinda,  alisema nchi ya Korea Kusini ilikuwa nchi masikini kama sisi kwa kipindi cha miaka ya nyuma ila nchi hiyo kwa sasa ipo juu kwenye masuala ya kiuchumi ukilinganisha na nchi yetu ambayo ina madini na rasilimali nyingi.

“Korea Kusini suala kuchelewa chelewa  kama sisi hawana, wao wanajali sana muda na hakuna kitu mali kama muda, muda ni mali kuliko kitu chochote,”alisema na kuongeza kuwa

“Wanafanya kazi kwa nidhamu hata mwendo wao ni wa nidhamu tofauti na sisi tunatembea muda wote kama tumechoka,”

 Naye, Mwanzilishi na Rais wa Chingu Kota Centre, Andrew Dyson Bukuku alisema taasisi hiyo itakuwa kituo kitakachoshughurikia  vyuo  Vikuu kutoka nje ya Tanzania na ndani ya Tanzania kwaajili ya kuwaelimisha watu utamaduni wa korea.

“Kwa mfano Korea ukikuta bomba limepasuka, wanapiga ngoma watu wote watatoka kwaajili ya kuja kusaidiana kulitengeneza ila kwa sisi hapa ukikuta hivyo utaacha na kusema maji si ya Dawasco hayo,”alisema

Kwa upande wake Project Manager  Nasibu Koko, alisema Chingu Kota Centre iliazishwa kwa lengo la kuwaweka wadau wa maendeleo na tamaduni za Asia na Tanzania.

“Na katika nchi za Asia tumeaza  na  Korea Kusini kwani  uchumi wake ulikuwa sawa sawa na nchi za Afrika lakini leo hii nchi hiyo ni moja kati ya nchi zenye uchumi mkubwa dunia,”

Aidha Mkutano huo wa siku tatu ulihudhuriwa na wanafunzi kutoa  Chuo cha Amity Haryana kilichopo India, Profesa Kumari Mansi na Kunal Anand pamoja na Dokta Sabine Burghart kutoka Chuo cha Vienna.

Picha ya Pamoja na Spika wa Bunge Mstaafu Anne Makinda baada ya kufungua mkutano huo jana jijini Dar es Salaam.



 Rais na  Mwanzilishi wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Chingu  Kota, Andrew  Bukuku katika picha ya pamoja na wageni wake wa ndani na kutoka Korea Kusini na China.

Spika  Mstaafu, Anne Makinda (wa pili kulia) akimsikiliza Profesa, Geofrey Calimag kutoka Korea akizungumzawakati wa Mkutano wa kujadili utamaduni wa Korea Kusini na nchi zingine za Asia uliowahusisha wanafunzi wa vyuo vikuu Jijini Dar ea Salaam mei 25, 2017, kulia ni Rais na  Mwanzilishi wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Chingu  Kota, Andrew  Bukuku na kushoto ni Mweka hazina wa Taasisi hiyo, Pamela Bukuku 
 Rais na  Mwanzilishi wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Chingu  Kota, Andrew  Bukuku (kulia) akizungumza  wakati wa Mkutano wa kujadili utamaduni wa Korea Kusini na nchi zingine za Asia uliowahusisha wanafunzi wa vyuo vikuu Jijini Dar ea Salaam mei 25, 2017. kushoto ni  Profesa, Geofrey Calimag kutoka Korea na Spika  Mstaafu, Anne Makinda.

(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA).

Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.