RAIS DKT MAGUFULI APOKEA KWA MASIKITIKO VIFO VYA WANAFUNZI 32, VILIVYOTOKEA KWA AJALI ARUSHA.


KAMANDA WA POLISI ARUSHA 

Na Mwandishi Wetu.

WANAFUNZI 32, walimu wawili na derava mmoja wa Shule  Lucky Vincent Nursery & Primary  iliyopo Arusha, wamefariki dunia baada ya Coastar waliyokuwa wakisafira kupinduka eneo la mlima Rock Wilaya ya Karatu.

Akizungumzia ajali hiyo  leo , Kamanda wa Polisi, mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema Costar hiyo yenye Namba za usajili T. 781 iliyokuwa imebeba abiria zaidi ya 38 iliyokuwa ikitokea Arusha imepinduka na kusababisha vifo vya watu 35  huku watano wakiwa mahututi.

Kamanda Mkumbo, alisema katika ajali hiyo wanafunzi 32 na watu wazima watatu wakiwamo walimu wawili  na dereva mmoja  wamefariki  dunia katika ajari hiyo.

Pia alisema bado wanaendelea kuchunguza chanzo cha ajali hiyo pia, huku akisema hali za mahututi sio nzuri. 

Muonekano wa gari aina ya Coastar iliyokuwa imepakia wanafunzi wa  Shule  ya  Lucky Vincent Nursery & Primary  iliyopo Mkoani Arusha.
 Baadhi ya Miili ya wanafunzi hao iliyotolewa eneo la Rhotia  Marera baada ya basi hilo kuacha njia na kutumbukia korongoni.

Baadhi ya wananchi walioenda kushuhudia ajali hiyo wakishuhudia uokoaji wa maiti hizo.


Comments

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.