Posts

Showing posts from April, 2017

WATANZANIA WATAKIWA KUWA WAVUMILIVU NA SIO KUTAFUTA NJIA YA MKATO.

Image
  Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam WATANZANIA, wametakiwa kuwa wavumilivu kwa jambo lolote wanalolifanya na sio kutafuta njia za mkato kufikia malengo yao ambazo zitawafikisha pabaya. Wito huo umetolewa leo na Askofu  Mkuu wa Dayosisi Kuu ya Dar es Salaam na Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania (KMUT), Emmaus Mwamakula,  katika kituo cha Ibada cha Mliman City Worship Centre (MCC). “Watanzania tuwe wavumilivu na sio kutafuta njia za mikato kwenye maisha yetu kwani jambo lolote lile jema  hufanywa kwa bidii na sio kutumia njia za mkato,”alisema na kuongeza “Tujifunza uvumilivu kama neo   la leo lilivyosema, tuogope mambo ya mkato kwani mambo haya yatatupeleka mahali pasipo pazuri,”   “Mfano katika nchi yetu siku hizi   za karibuni Rais Dkt. John Pombe Magufuli alikabidhiwa Ripoti   na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) na kubaini   mambo mbalimbali ikiwamo baadhi ya watumishi wa umma kugushi vyetu   na walifanya haya kwa kupitia njia ya mkato ili waweze kufik

WAJAWAZITO WATAKIWA KUWAHI HOSPITALI WANAPOONA DALILI ZA KUJIFUNGUA.

Image
Na Ramadhani Ali/Maelezo Zanzibar .                         MAMA wajawazito wameshauriwa  wanapoonyesha dalali za kuwa tayari kujifungua wanatakiwa kuwahishwa Hospitali ama vituo vya afya mara moja bila ya kupewa dawa za aina yoyote majumbani kwani ni hatari kwa afya zao. Mwenyekiti wa Baraza la Wakunga na Wauguzi Zanzibar, Amina Abdulkadir Ali, ameeleza hayo katika mkutano na  waandishi wa  habari ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Wakunga Dunia katika Ukumbi wa Wizara ya Afya Mnazimmoja Zanzibar. Alisema kumuwahisha mzazi katika kituo cha afya mapema kunarahisisha kupata huduma kwa haraka na iwapo anatatizo linalomkabili kujulikana mapema na kupatiwa ufumbuzi katika hatua za awali. Amina alisema  huduma za mama wajawazito na watoto wachanga zimeimarishwa katika vituo vingi vya afya vijijini na hakuna haja kwa mama wajawazito kulazimisha kujifungulia Hospitali kuu ya Mnazimmoja. Amewashauri kuvitumia vituo vya afya vilivyokaribu nao na iwapo kutatokea tatizo kubw

RAIS DKT MAGUFULI ALIVYOPOKELEWA KWA SHANGWE NA NDEREMO MKOAN KILIMANJARO.

Image
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Kmnda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Hamisi Issa alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017  Rais Dkt. Magufuli akilakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017  Rais Dkt. Magufuli akilakiwa na Waziri Mkuu , Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumam

NEMC YAWATOZA FAINI YA SH. MILIONI 20 WAWEKEZAJI WA KILIMO NA MIFUGO.

Image
Na Mwandishi Wetu, Kilolo BARAZA   la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), imewatoza faini ya jumla ya sh. milioni 20 wawekezaji wawili wa kilimo na ufugaji Wilayani Kilolo kwa makosa ya kuendesha shughuli zao bila kufanya tathmini ya uharibifu wa mazingira. Adhabu hiyo imetolewa na mwanasheria wa NEMC, David Kongola baada ya kutembelea mashamba ya wawekezaji hao na kubaini kasoro kubwa za kimazingira na kuhatarisha usalama wa vyanzo vya maji. Kongola alisema kuwa “Sasa adhabu yao hawa  sisi tunatoza Mil.10 kwa kila mmoja kwa kufanya hii shughuli bila ya kuwa na (IAA) Certificate na hiyo ipo wazi kwamba kifungu no.184 kinasema isizidi Mil.50 na sisi tun asema kwamba Mil.10 na tutawaletea invoice kwa kuendesha biashara yako bila ya kuwa na cheti cha tathimini ya mazingira.”alisema Kongola Adhabu ya NEMC imeyakumba mashamba ya mifugo ya Tomy Dairies na  la Ndoto yaliyopo kwenye kata ya Ihimbo ambapo mwanasheria wa NEMC alisema sheria lazima zifuatwe k

OFISA MISITU KILOLO,ASHINDWA KUDHIBITI VYANZO VYA MAJI.

Image
Na Mwandishi Wetu, Kilolo OFISA  Misitu wa  Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa ,Eugen Mwilafi, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kushindwa kutoa ufafanuzi wa kutosha kwa nini halmashuri hiyo imeshindwa kudhibiti kilimo kwenye vyanzo vya maji. Hali hiyo imetokana na kukithiri kwa kilimo cha mabondeni maarufu kama vinyungu kando kando ya mito ya Mtitu na Lukosi inayotiririsha maji kwenye mito ya Ruaha Mdogo na Mkubwa.  Ongezeko la kilimo cha vinyungu wilayani kilolo limebainishwa pia na viongozi wa wilaya hiyo mbele ya wajumbe wa kikosi kazi cha kuokoa ikolojia ya mto Ruaha Mkuu iliyoundwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu hivi karibuni wakati akiwa mkoani Iringa. Akizungumza Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Asia Abdallah, alisema inatakiwa wanaolima kwenye vinyungu kutolewa kwenye eneo hilo na kupelekwa kwenye ufugaji wa samaki au watafute maeneo mengine ambayo yanafaa kwa shughuli za uzalishaji mali. Wajumbe wa kikosi hicho walishuhudia mahindi yakiwa kat

WENYE VIWANDA IRINGA WAIOMBA SERIKALI KUWAPUNGUZIA TOZO ZA KODI.

Image
Na Mwandishi Wetu, Iringa BAADHI  ya wafanya biashara wenye viwanda mkoani Iringa wameiomba serikali kutazama baadhi ya kodi na tozo mbalimbali wanazotozwa ili kuviwezesha viwanda kuzalisha kwa ufanisi ili kuleta ushindani. Hayo yamebainishwa na baadhi ya wamiliki wenye viwanda mkoani Iringa wakati mwenge wa uhuru ulipopita kuzindua miradi yao ambapo ukiwa kwenye kiwanda cha nyanya cha dabaga katika halmashauri ya wilaya ya kilolo.  Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Petronila Alphonce alimweleza kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Amour Hamad Amour kuwa kutokana na tozo hizo baadhi ya bidhaa imekuwa ni ngumu kushindana sokoni.  Ukiwa kwenye kiwanda cha kuzalisha nguzo za umeme cha Agora kilichopo katika Halmashauri ya Iringa Vijijini mwenge huo ulizindua kiwanda hicho kinachozalisha nguzo za umeme ambapo akitoa taarifa kwa kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa. Meneja wa kiwanda hicho Edger Edson alisema pamoja na kuzalisha nguzo zenye ubora kiwanda hicho hakina

WANANCHI KIJIJI CHA MALIZANGU WAIOMBA SERIKALI KUWABORESHEA MIUNDOMBINU YA SKIMU YA UMWAGILIAJI.

Image
Na Mwandishi Wetu, Iringa WANANCHI wa Kijiji cha Malizangu Kata ya Mlowa Wilaya ya Iringa wameiomba serikali kuwajengea miundombinu ya skimu za umwagiliaji iliwaweze kuboresha kipato na uhakika wa chakula. Wakizungumza na mwandishi wa blog hii kwa nyakati tofauti, kijijini hapo walisema kuwa mazao ambayo  walitarajia kuvuna msimu huu yamekauka baada ya mvua kuacha kunyesha. “kilimo cha kutegemea mvua hakina uhakika tunaoimba serikali itujengee miundombinu ya skimu za umwagiliaji ili tuweze kuboresha kipato na uhakika wa chakula,”alisema Nae, Marian Kamugishi, alisema kata hiyo mvua zimekuwa za shida,watu wanajuhudi za kulima lakini miundombinu hususani maji ya umwagiliaji hawana hivyo wanalima kilimo cha kubahatisha. “Kilimo hiki hakina maana,tunadhani mkombozi wetu ni pale tunapopata maji ya umwagiliaji mfano skimu au tukavuna maji ya mvua kupitia mto mlowa na hali ya uchumi imekuwa ngumu kutokana na mvua kutokunyesha,”alisema Kamugishi alisema kiujumla ki