CHAMA CHA MADEREVA “BAJAJI” KIMEIOMBA SERIKALI KUTOTOA LESENI KWA MADEREVA WASIO NA SIFA.

Mwenyekiti wa chama cha Maendeleo ya Madereva Pikipiki Matairi Matatu Tanzania, Edward Mwenisongole akizungumza na madereva hao leo baada ya mgeni rasmi  Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Ofisi ya Mkoa wa Polisi Kinondoni, Samson J. Nguno, kuwasili katika mkutano huo.

 Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Ofisi ya Mkoa wa Polisi Kinondoni, Samson J. Nguno, akisaini kitabu cha wageni baada ya kufika.

 Wageni kutoka  Kampuni ya Shinyanga Emporium  na wauzaji wa pikipiki na bajaji aina Piagio, waliofika kwenye mkutano huo leo jijini Dar es Salaam kwaajili ya kutoa elimu ya fursa juu ya mikopo ya bajaji na pikipiki.

 Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Ofisi ya Mkoa wa Polisi Kinondoni, Samson J. Nguno, akimkabidhi cheti  mmoja wa madereva wa bajaji waliohitimu mafunzo hayo ya wiki mbili na kutunukiwa vyeti leo. 

 Madereva wa bajaji waliotunukiwa vyeti leo wakinyoosha mikono baada ya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Ofisi ya Mkoa wa Polisi Kinondoni, Samson J. Nguno, kuwataka kunyoosha mikono watu walioshiriki mafunzo hayo na ambao watatunukiwa vyeti hivyo.

Madereva wakishangilia baada ya Mwenyekiti wa chama hicho, Edward Mwenisongole kusema  madereva ambao hawana sifa za udereva hawatapewa leseni.

 Meneja Masoko wa Kampuni ya Shinyanga Emporium  na wauzaji wa pikipiki na bajaji aina Piagio, Herman Bernard, akizungumzia jinsi kampuni hiyo inavyotoa mikopo hiyo ya bajaji na pikipiki.

 Madereva bajaji wakifuatilia ugawaji wa vyeti hivyo leo.


 Meneja Masoko wa Kampuni ya Shinyanga Emporium  na wauzaji wa pikipiki na bajaji aina Piagio, Herman Bernard ,akionyesha moja ya bajaji ambazo zinakopeshwa na kampuni hiyo.

 Madereva bajaji waliotunukiwa vyeti vya mafunzo ya udereva leo.

Meneja Masoko wa Kampuni ya Shinyanga Emporium  na wauzaji wa pikipiki na bajaji aina Piagio, Herman Bernard, akizungumza na mmoja wa madereva pikipiki ambaye alihitaji ufafanuzi juu ya mikopo inayotolewa na kampuni hiyo.

(PICHA ZOTE NA MAISHA NI HABARI). 


 Na Enles Mbegalo

CHAMA cha Maendeleo ya Madereva Pikipiki Matairi Matatu Tanzania kimeiomba serikali kutotoa leseni kwa  madereva ambao hawana sifa za udereva ili kuepuka ajari ambazo zinawaacha madereva vilema.

Ombi hilo limetolewa leo jijini Dar es Salaam  na Mwenyekiti wa chama hicho, Edward Mwenisongole wakati akisoma risala kwa mgeni rasmi wakati wa tukio la kukabidhi vyeti kwa madereva 110 waliohitimu mafunzo ya udereva.

“Tunapendekeza madereva wote ambao hawana sifa za udereva wasipewe leseni na wale ambao wanaleseni lakini hawajapata mafunzo ili kuepuka ajari ambazo zinawaacha madereva wengi vilema,”alisema

Mwenisongole, alisema dhamira kuu ya chama chao ni kuhakikisha madereva wote wa pikipiki wanapata maendeleo katika nyanja kuu mbili ikiwamo kiuchumi na kijamii na kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika kukuza uchumi wa taifa na kulipa kodi.

“Changamoto kubwa ni mwitikio wa madereva wengi kupata mafunzo umekuwa mdogo hii ni kutokana na utamaduni ulio kuwa umejengwa siku za nyuma madereva kupata leseni bila kupitia mafunzo ya udereva kwenye chuo kinachotambulika na serikali,”alisema Mwenisongole.

Naye, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Ofisi ya Mkoa wa Polisi Kinondoni, Samson J. Nguno aliwataka madereva hao kutoendesha bajaji wakiwa wamelewa  ili kupunguza ajari za mara kwa mara na pia amewataka kuheshimu sheria za barabarani.

Nguno aliwataka madereva hao, kuwafichua waharifu wanaopora kwani wamekuwa wakitumia vyombo hivyo.

Kwa upande wake, Meneja Masoko wa Kampuni ya Shinyanga Emporium  na wauzaji wa pikipiki na bajaji aina Piagio, Herman Bernard alisema kampuni hiyo inatoa elimu ya fursa ya mikopo kwa wajasiriamali  na waendesha Bajaji na Pikipiki.

Herman alisema kuwa bajaji aina ya Piagio inakopeshwa kwa Sh. Milioni 6.9 ambayo italipwa kwa miezi 18.






Comments

  1. Ni vizuri sana nimeipenda ila swali langu ni kwanini hamjanialika? mnikumbuke nami nina jambo ambalo ningeongeanao naomba ikitokea tena mnialije niwasikilize pamoja nakuchangia mada.
    Ahsante.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SERIKALI YAREJESHA KAMBI TANO ZA JKT ZILIZOKUWA ZIMESITISHA MAFUNZO YA JESHI.

BELENG’ANYI, MBUNIFU MWENYE MALENGO YA KUTENGENEZA MGODI WA KUFUA UMEME.