BUNDU, MBUNIFI WA SIMU YA "KIFUU"AMBAYE HAKUNUFAIKA NA KAZI YAKE.
Bundu, akiwa na vitu vingine alivyobunia ambavyo ni kobe wakieletroni pamoja na simu yenye umbo la ndege mnyama. Peter Akaro. ALLY Bundu ni kijana ambaye ana jishughulisha na ubunifu kwa kipindi kirefu, ingawa kwasasa amekata tamaa kutokana na mambo aliyokutana nayo katika kazi za ubunifu. Kabla ya hayo, Bundu amebuni Simu ya Mezani ya Kifuu cha Nazi, hii simu ni kwaajili ya kudhibiti upotevu wa simu kadi (hasa kwa kipindi cha nyuma ambapo kulikuwa hakuna huduma ya kurejesha simu kadi). Simu hii ya kifuu inaweza kutumikia wakati haina simukadi (laini), pengine mtumiji ameificha sehemu isiyoweza kuonekana na wezi, na mtumiaji anaweza kuwasiliana bila matatizo yoyote ya kimtandao. Vitu vilivyo unda simu. Anasema kitu cha kwanza ni kifuu cha nazi kama kava la nje, kandambili kwaajili vibonyezeo (baton), wayaza ‘transformer’, kioo (display) cha simu ya Motorola, kadi ya deki ya runinga (simsung) kwaajili ya kunukuu mtandao (network). “Kadi ni kwaajil...