Posts

MAMA JANETH MAGUFULI AZUNGUMZA NA KUTOA MISAADA MBALIMBALI KWA WAZEE WASIOJIWEZA 400 CHATO MKOANI GEITA

Image
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na Mwakilishi wa Wazee 400 kutoka Wilaya ya Chato Bi. Winfrida Lawrent(65) kutoka Kata ya Kasenga kabla ya kuwakabidhi msaada wa vyakula mbalimbali ikiwemo Kilo 10,000 za Mchele, Kilo 10,000 za Unga wa mahindi, Kilo 4000 Maharage, Mafuta, Sabuni pamoja na Sukari. Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na Mwakilishi wa Wazee 400 kutoka Wilaya ya Chato Bw. AnatoryBisate (64) kabla ya kuwakabidhi msaada wa vyakula mbalimbali ikiwemo Kilo 10,000 za Mchele, Kilo 10,000 za Unga wa mahindi, Maharage kilo 4000, Mafuta, Sabuni pamoja na Sukari. Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwakabidhi kwa pamoja mafuta waakilishi wa Wazee kutoka kata ya Kasenga AnatoryBisate (64) kulia pamoja na Bi. Winfrida Lawrent(65) kushoto mara baada ya kuzungumza na wazee 400 katika Ukumbi wa Mshikamano SACCOS Chato mkoani Geita. Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiimba pamoja na wanakwaya wa Mwagazege mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mshik...

SOMA MAGAZETI YA ALHAMIS LEO, JULY 6,2017.

Image

MAHAKAMA YAMFUATA MANJI HOSPITALI, ASOMOMEWA MASHTAKA YA UHUJUMU UCHUMI

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana imelazimika kuhamishia shughuli zake katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa muda kumsomea mfanyabiashara Yusufali Manji (41), mashitaka ya uhujumu uchumi yanayomkabili. Manji amesomewa mashtaka hayo katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo Hospitalini hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mhe. Huduma Shaidi. Katika kesi hiyo, Manji anashitakiwa pamoja na wenzake watatu, Meneja Rasilimali watu wa Kampuni ya Quality Group Ltd, Deogratius Kisinda (28), Mtunza stoo, Abdallah Sangey (46) na Thobias Fwere (43)  mkazi wa Chanika, ambapo wote watatu wamesomewa mashtaka yao katika Mahakama hiyo kabla haijahamia hospitali ya Muhimbili kuanzia muda wa saa Tisa alasiri na kumalizika saa 16:41 (saa kumi na dakika arobaini na moja). Mahakama ilifikia uamuzi wa kuhamia Muhimbili baada ya Manji kuwa amelazwa Hospitalini hapo akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo na kulazimika kusomewa mashtaka yake akiwa kitandani. Akisoma mashtaka hayo, wakili Mwanda...

SOMA MAGAZETI YA JUMATATU LEO, JULY 3,2017.

Image